• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

UFUNGUZI WA MAFUNZO YA UPELELEZI NA UENDESHAJI WA KESI ZA WANYAMAPORI NA MISITU


Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi ameitaka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuhakikisha upelelezi wa makosa ya Jinai kuhusiana na misitu na wanyamapori unaratibiwa vizuri, watuhumiwa wanafikishwa mahakamani na Mashtaka yanaendeshwa kwa ufanisi mkubwa kwa lengo la kutokomeza ujangiri, kulinda rasilimali zetu na kuikuza sekta ya utalii na uhifadhi nchini. "Ninafurahi kuona mafunzo haya ninayofungua leo yamejumuisha wadau wote muhimu katika mfumo wa upelelezi na Uendeshaji wa makosa ya Jinai yahusuyo misitu na wanyamapori. Hivyo, sina shaka kwamba, mafunzo haya yatakuwa chachu ya mabadiliko na mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya ujangiri na ulinzi wa maliasili zetu." Akizungumza hayo Profesa Kabudi wakati akifungua mafunzo ya upelelezi na Uendeshaji wa Kesi za wanyamapori na misitu yanayofanyika Mkoani Morogoro katika Ukumbi wa Nashera Hotel.

baadhi ya washiriki 


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mashtaka nchini ameeleza kwamba kumekuwa na ongezeko la makosa ya wanyapori na mazao ya misitu nchini hivyo mafunzo haya kwao yana tija katika kulinda maslahi ya Taifa. Akifafanua ukubwa wa tatizo hilo, Bw. Mwakitalu amesema kuwa katika kikao cha Mahakama ya Rufaa kilichoanza leo tarehe 18 Oktoba, 2021 Musoma mkoani Mara, imebainika kuwa kuna kesi 18, ambapo kesi 14 kati ya hizo ni za wanyamapori na misitu. 



Naye Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Makosa ya Mazingira na Maliasili wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka,
 Rosemary Shio alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo na kuwapatia ujuzi utakao wawezesha kupeleleza na kuendesha kesi za wanyamapori na misitu kwa weledi na uadilifu







 

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .