• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

TCRA YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA

 Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekabidhi vifaa vya TEHAMA kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa lengo la kuongeza ufanisi wa kazi zikiwemo kompyuta Mpakato 11, kompyuta za mezani 5, Mashine ya kunakilia 1 na Mashine ya kuchapia (Printa )1.

Akikabidhi vifaa hivyo katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka leo Jijini Dodoma Mkurugenzi wa Sheria kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Modestus Ndunguru  ameitaka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuvitumia vifaa hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili vikalete tija na mchango mkubwa kwa Watanzania.

“Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania inafarijika sana inapotoa vifaa hivi kwa Taasisi lakini faraja ni kubwa zaidi hicho kinachotolewa kinapata Thamani kubwa kutokana na mchango wa mtumiaji.Ofisi ya Mashtaka ndiyo itakayoleta thamani ya vifaa hivyo kwa Jamii, nendeni kavitumieni vifaa hivi kwa huduma nzuri ili mafao yafike kwa jamii." Amesema Modestus Ndunguru.


Aidha, Nduguru Amesema katika Kompyuta Mpakato 11 watakabidhi Kompyuta Mpakato 5 na kubakia Kompyuta Mpakato 6 ambazo zitakabidhiwa muda mfupi ujao ambapo amesema wataendelea kutoa vifaa vya TEHAMA kwa Taasisi mbalimbali nchini ili kuongeza ufanisi na urahisishaji wa kazi.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande ameihakikishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kwamba vifaa hivyo vitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na vitatunzwa kwa kila namna ili vikalete matokeo chanya katika kuwahudumia Watanzania.

“Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kama zilivyo ofisi zingine za haki jinai zina mahitaji makubwa ya vifaa vya TEHAMA. Mikoa ya Kimashtaka Tanzania ipo 30 na inahitaji vifaa vya TEHAMA, ninaahidi kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kwamba vifaa hivi  vitaenda kutumika vizuri lakini pia kutokana na uhitaji mkubwa wa vifaa hivi kesho vinaenda kutumika na havitokaa stoo kwa sababu mahitaji yake ni makubwa” amesema  Bw.Joseph Pande.

Ikumbukwe kuwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeanzishwa kama Ofisi huru ya Umma kupitia Tangazo la Serikali na 49 la Mwaka 2018 la tarehe 13 February 2018 la kuanzisha Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa ajili ya kutekeleza Mamlaka ya kikatiba aliyopewa Mkurugenzi wa Mashtaka ya kusimamia haki jinai kwa Mujibu wa Ibara ya 59B ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977

Share:

MAAFISA TRA NA BENKI WALIOACHIWA HURU NA MAHAKAMA YA KISUTU WATIWA HATIANI KWA KOSA LA UTAKATISHAJI FEDHA

 Mahakama ya Rufani imetoa hati ya kuwakamata na kuwaweka  rumande washtakiwa wanne, akiwamo aliyekuwa mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Idara ya wafanyabiashara wakubwa anaefahamika kwa jina la Justice Katiti.                                     

Awali, wajibu rufani walishtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu katika kesi ya jinai namba 152 ya mwaka 2010 kwa mashtaka kumi, yakiwamo kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu. 

Washtakiwa hao wanadaiwa kula njama ya  kufanya uhalifu, kuwasilisha nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya Udanganyifu kiasi cha shilingi milioni 338 na utakatishaji fedha haramu.

Mahakama hiyo imewatia hatiani washtakiwa hao,  baada ya kutengua uamuzi wa hukumu iliyotolewa na Mahakama kuu Kanda ya Dar es salaam ya kuwaachia huru washtakiwa hao, baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao.

Mbali na Katiti, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya rufani ya Namba 15/2018 ni Robert Mbetwa na Gidion Otullo, waliokuwa wafanyabiashara na Godwin Paula. Na jopo la Majaji watatu wa Mahakama hiyo, wakiongozwa na Shabani Lila, Ignas Kitusi na Lilian Mashaka, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutolewa uamuzi.

Katika uamuzi huo, jopo hilo la majaji limeamuru wajibu rufani wawekwe mahabusu huku jalada la kesi hiyo, likielezwa kurejeshwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kutoa adhabu.

Awali, jopo la Mawakili wa Serikali Waandamizi watatu  likiongozwa na Nassoro Katuga, Hellen Moshi na Tumaini Mafuru,  walidai Serikali ilikata rufaa baada ya kutoridhika na hukumu iliyotolewa Mahakama ya Kisutu na Mahakama Kuu.

Share:

USHIRIKIANO WA TAASISI TATU UMETUPA MATOKEO CHANYA - DPP


Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Sylvester Mwakitalu ameeleza namna jinsi ambavyo Ofisi yake ilivyoshirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai katika kupunguza kesi mbalimbali zinazotokana masuala ya jinai. 

                                                


"Uhalifu hauwezi kuisha kwa taasisi moja kupambana peke yake, lakini tukishirikiana kwa pamoja tunaweza kukabiliana na uhalifu. Na kwa taarifa tulizonazo tumefanya vizuri. Ushirikiano wa hizi Ofisi tatu umetupa matokeo chanya, kwa sasa Upelelezi na uchunguzi wa makosa ya jinai unafanyika vizuri, mashtaka yanaendeshwa vizuri na matokeo tunayaona." Amezungumza hayo Mkurugenzi wa Mashtaka wakati akifanya mahojiano na Waandishi wa vyombo vya habari mara baada ya kufungua kikao cha Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ambacho kimefanyika leo tarehe 11 Agosti, 2022 katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gaspar Jijini Dodoma

Pia DPP aliendelea kueleza kuwa kikao hicho ni muhimu kwa maana kinalenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu  ya kipindi cha mwaka uliopita pamoja na kuweka mikakati ya utendaji wa mwaka unaofuata na pia nikwa namna gani watashirikiana kwa pamoja kukabiliana na uhalifu.

                                                          


Aidha, Mwakitalu alisema kuwa Takwimu walizonazo kwa sasa mahabusu wengi sana wamepungua kwenye magereza, na wamepungua kwasababu kesi zao zinakuwa zimefika mwisho kwa maana kuwa wamefungwa au Mahakama imewakuta hawana hatia na kuweza kuwaachia huru. Hivyo kupitia tathmini hiyo iliyofanyika na taarifa zilizopo kazi inafanyika vizuri.

Nae pia Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Kamishna wa Polisi Salum Hamduni alieleza kuwa kikao hicho ni mwendelezo wa kikao cha mwaka jana ambacho walikaa na wadau katika mnyororo wa haki jinai, hususani katika taasisi hizo ambazo zinahusika na uchunguzi na uendeshaji wa mashtaka. Na lengo la vikao hivyo ni kuhakikisha kwamba wanafanya kazi kwa pamoja katika kuhakikisha wanatoa huduma ambayo wananchi waliitarajia

"Sisi tunalenga haki za watu, kwahiyo pale ambapo tunachelewa kukamilisha upelelezi maana ake tunachelewesha haki za mtu mwingine." Amezungumza hayo Mkurugenzi Hamduni.

Pia Kamishna wa Polisi Salum aliendelea kueleza kuwa lengo kuu hasa la vikao hivyo ni kuona namna ambavyo wanaweza kuongeza tija ya ufanisi katika kuharakisha shughuli za upelelezi na uendeshaji wa mashtaka.             

Hivyo basi kupitia ushirikiano huo na uratibu ambao unafanywa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imekwenda kupunguza kwa kiwango kikubwa manung'uniko ya wananchi. Pia tathmini itakayofanyika itasaidia kuona namna ambavyo wamefanya vizuri na wapi wamekwama ili kuweza kurekebisha na hatimae kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi ambao wanawahudumia

Aidha, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishna wa Polisi  Ramadhani Kingai ameeleza kuwa kikao hicho kina dhumuni la kuangalia ni wapi ambapo wamefikia kulingana na yale waliyoelekezana katika maazimio ya kikao kilichopita cha mwaka jana mwezi Julai. Na pia kuangalia ni wapi kuna mapungufu ili kuweza kuboresha kwa lengo la kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma bora na kupunguza malalamiko katika jamii yanayohusiana na utendaji wao wa kazi ikiwepo upelelezi kuchukua muda mref                               

"Tumefanya kaguzi ili kubaini mapungufu haya, na sasa tupo kwenye kikao hiki ili kuweza kufanya tathmini ni kwa namna gani tunaweza kuyamaliza mapungufu haya." Amezungumza hayo Kamishna Kingai

Pia aliendelea kueleza kuwa suala la uchunguzi kuchukua muda mrefu kunatokana na sababu mbalimbali za kiutendaji, lakini kulingana na sasa muungano wao unapunguza hizo changamoto                                      




Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .