• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

WAZIRI NDUMBARO AELEZA UMUHIMU WA MWONGOZO

 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro  ameipongeza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa kushirikiana na wadau wengine mbalimbali wakiwepo Magereza, Polisi, TAKUKURU na Taasisi za Kifedha kwa kuzindua Mwongozo wa Ushirikiano wa Wadau katika Upelelezi wa Utakatishaji Fedha Haramu, Ugaidi na Ufadhili wa Ugaidi ambao wanapambana katika kuzuia makosa hayo makubwa ambayo yanapangwa na kuvuka mipaka.

Katika uzinduzi huo uliofanyika tarehe 24 Mei, 2023 Jijini Dodoma Waziri Ndumbaro ameeleza kuwa Mwongozo huo ni muhimu sana kwani unachangia katika kuwaleta wadau mbalimbali pamoja ili juhudi zao za kudhibiti makosa hayo makubwa matatu ambayo ni Utakatishaji Fedha, Ufadhili wa Ugaidi na Ugaidi wenyewe viweze kufanyika kwa pamoja kwa kuwa makosa hayo ni makosa ambayo ni hatari sana, makubwa na ni makosa ambayo yanapangwa.

Aidha, Mhe. Ndumbaro amemesema kuwa umuhimu wa Mwongozo huo pia utasaidia kupata namna bora ya kushirikiana na nchi nyingine mbalimbali duniani zikiwepo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Sadic,  Afrika na Duniani kote.

"Mtu yeyote anaweza akafanya uhalifu wowote na kujipatia fedha zinazotokana na uhalifu huo na anaweza kuzitumia fedha hizo na kuziweka katika nchi nyingine. Hivyo kwa kuweka ushirikiano huo tunaweza kumkamata mhalifu huyo na kupata ushahidi wake katika nchi husika alikowekeza fedha hizo na kuchukua jukumu la kutaifisha mali zake na kuwa mali za Serikali. Ni jambo ambalo litasaidia kuondosha uhalifu wa namna hiyo katika jamii yetu." Amefafanua hayo Waziri Ndumbaro.

Mwongozo huu pia unalenga katika kukuza ushirikiano pamoja na kuwajengea uwezo wadau wote hususani kwa jamii kwani ndio wadau namba moja ili waweze kufahamu juu ya jambo husika linaloendelea katika jamii husika.



Share:

DPP AZINDUA MWONGOZO WA USHIRIKIANO WA WADAU KATIKA UPELELEZI WA UTAKATISHAJI FEDHA HARAMU, UGAIDI NA UFADHILI WA UGAIDI.

 Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Sylvester Mwakitalu amezindua Mwongozo wa Ushirikiano wa Wadau katika Upelelezi wa Utakatishaji  Fedha Haramu, Ugaidi na Ufadhili wa Ugaidi kwa lengo la kudhibiti na kupambana na makosa hayo.



Uzinduzi huo umefanyika tarehe 24 Mei, 2023 Jijini Dodoma, ambapo katika uzinduzi huo Mkurugenzi Mwakitalu ameeleza kuwa Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia yamewarahisishia wahalifu kufanya makosa mbalimbali bila kutambulika zaidi, hivyo kupitia Mwongozo huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti uhalifu huo.

"Leo Tumezindua Mwongozo wa namna ambavyo Taasisi zinazohusika na mapambano dhidi ya makosa hayo jinsi zitakavyoshirikiana na kuratibiwa vizuri kwa shuguli zote zinazohusiana na makosa ya uhalifu wa namna hiyo. Na ushirikiano ya Taasisi hizi ni zile Taasisi za Uchunguzi, Taasisi za Usimamizi wa Sheria na Taasisi zingine za kifedha." Amefafanua hayo Mkurugenzi Mwakitalu.

 Aidha, DPP ameeleza kuwa Mwongozo huo utaziongoza Taasisi hizi ambazo zitaratibiwa vizuri, na taarifa za uhalifu zitakazopatikana ni namna gani zitapelekwa kwenye chombo kingine ambacho chenye Mamlaka ya kuweza kuzishughulikia,  kuzichunguza na namna ambavyo zitafika kwenye hatua ya Mashtaka kama makosa hayo yatathibitika kwamba upo ushahidi wa kutosha wa kuyaendesha Mahakamani.

Mkurugenzi Mwakitalu amezisihi Taasisi kushirikiana kwa pamoja ili muhalifu anapofanya kosa asije akatoka bila kuguswa na mkono wa sheria.

"Makosa haya yapo na tunazo kesi nyingi Mahakamani ambazo zipo zinaendelea katika hatua mbalimbali na wapo watu ambao tunawashtaki kwa makosa ya Utakatishaji Fedha, lakini pia tunazo kesi za ugaidi zinaendelea katika hatua mbalimbali Mahakamani." Amesema Mwakitalu.

Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Bw. Aretas Lyimo amesema Madawa ya Kulevya ni eneo moja wapo ambalo linatumika sana katika utakatishaji Fedha na Ufadhili wa Ugaidi, hivyo Mwongozo huo utasaidia kuunganisha nguvu ya pamoja katika kupambana na Uhalifu hapa nchini.

"Mwongozo huu utatusaidia sana kupunguza makosa mbalimbali ya kiuhalifu hususani Makosa ya Kupangwa ambayo Taasisi zetu zinashirikiana katika kuyafanyia kazi."  Amefafanua Jenerali Lyimo.

Utakatishaji fedha, Ugaidi na Ufadhili wa Ugaidi ni maeneo ambayo Serikali inaenda kuyadhibiti ili Taifa liendelee kuwa salama kwa watu wake.



Share:

WAHUKUMIWA BAADA YA KUKUTWA NA HATIA YA KUINGIZA MIFUGO NDANI YA PORI LA AKIBA.

 Picha za Ng'ombe waliotaifishwa na Mahakama ya Hakimu  Wilaya ya Same baada ya wahusika kuingiza mifugo hiyo kinyume cha Sheria ya Misitu Na 14 ya Mwaka 2002 katika pori la Akiba Chambogo.

Mahakama ya Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro imewahukumu  Elia Lemsumba, Moono Natetwa na Juma Hassan Omary baada ya kukutwa na kosa la kuingiza mifugo yao kinyume cha sheria katika pori la Akiba Chambogo.

Kesi hiyo ya jinai Na. 80 na 84 ya mwaka 2023 imetolewa hukumu mnamo tarehe 8 Mei, 2023 katika Mahakama hiyo  baada ya watuhumiwa kukutwa na hatia.

Awali wakisoma Mashtaka, Waendesha Mashtaka wa Serikali wakiongozwa na Flavian Kalinga na  Samwel  Magoko wamesema kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa hilo mnamo tarehe 26 Aprili, 2023 mwaka huu kwa kuingiza wanyama katika pori hilo kinyume cha sheria ya misitu Na. 14 ya mwaka 2002.Picha za Ng'ombe waliotaifishwa na Mahakama ya Hakimu  Wilaya ya Same baada ya wahusika kuingiza mifugo hiyo kinyume cha Sheria ya Misitu Na 14 ya Mwaka 2002 katika pori la Akiba Chambogo.

Watuhumiwa hao walikuwa wakikabiliwa na makosa matano ikiwemo kuingia hifadhini, kuingiza mifugo, kuharibu uoto wa asili, kuharibu na kuvuruga biolojia ya ndani ya hifadhi na Kujenga Makazi.

Akitoa hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Same Mhe. Mussa Hamza   amemuhukumu mshtakiwa Elias Lemsumba mwenye kesi ya jinai Na. 84/2023 adhabu ya kifungo cha miaka miwili  gerezani kwa makosa yote matano.

 Mshtakiwa Moono Natetwa  mwenye kesi ya Jinai Na.84/2023 amehukumiwa kulipa faini ya kiasi cha shilingi 1,500,000/= kwa makosa yote matano pamoja na  jumla ya ng'ombe 235 kutaifishwa na kuwa mali ya Serikali.Picha za Ng'ombe waliotaifishwa na Mahakama ya Hakimu  Wilaya ya Same baada ya wahusika kuingiza mifugo hiyo kinyume cha Sheria ya Misitu Na 14 ya Mwaka 2002 katika pori la Akiba Chambogo.

Mshtakiwa Juma Hassan Omary mwenye kesi Na.80 ya mwaka 2023 amehukumiwa kulipa faini ya kiasi cha shilingi 1,500,000/= kwa makosa yote matano. Sambamba na hilo jumla ya ng'ombe 150 na Punda  mmoja(1) wametaifishwa kuwa mali na  Serekali ili liwe fundisho kwa wengine wenye nia ya kufanya vitendo hivyo vinavyosababisha upotevu wa rasilimali za nchi.

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .