• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

WATUMISHI WA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA KWA KUTENDA HAKI.

 Wa Kwanza Kulia ni Mkurugenzi wa Divisheni ya Utenganishaji wa Shughuli za Mashtaka na Upelelezi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Tumaini Kweka akiwa pamoja na viongozi wengine katika hafla fupi ya kuwaaga watumishi waliohama vituo vya kazi na kuwakaribisha waliofika Mkoani Shinyanga July 22,2023.

Na Ofisi ya Mashtaka-Kahama Shinyanga.

Mkurugenzi wa Divisheni ya Utenganishaji wa Shughuli za Mashtaka na Upelelezi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Tumaini Kweka amewataka  Watumishi wapya kuwa makini kwa kujiepusha na vitendo vya rushwa kwa kuwa Shinyanga ni mojawapo ya Mikoa yenye vishawishi vingi hivyo wafanye kazi kwa weledi kwa kuongozwa na uadilifu, hofu ya Mungu, kwa kuwa ni jukumu lao  huku akiwataka kuongozwa na weledi na ufanisi ili kutenda haki iliyo na usawa kwa wananchi.

Bw. Kweka ameeleza hayo wakati akifungua halfa fupi ya kuwaaga waliokuwa Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiwemo waliojariwa na waliohamia Mkoani Shinyanga wa ofisi hiyo pamoja na kupata chakula cha jioni kiliyoandaliwa na Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga.

Mkurugenzi Kweka amesema kuwa kuajiriwa ni sehemu ya kuaminiwa kuwatumia wananchi hivyo jukumu lao ni kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano na kuhudumia  wananchi kwa kuzingatia weledi wa kazi yao na taaluma yao

Aidha Mkurugenzi Kweka ameeleza kuwa kazi hiyo ngumu na inavishawishi vingi hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kuzingatia miiko ya utumishi wa umma kwa kujiepusha na rushwa pamoja na kupindisha haki hali ambayo itasababisha kudhohofika kwa utendaji.

Bw. Kweka pia ameishukuru Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoani Shinyanga kwa kufanya kazi zake kwa kujituma na kuleta ufanisi katika kushughulikia mashauri ya kesi  mbalimbali ambapo wamefanya kazi kubwa na yenye kutukuka.

 “Miongoni mwa watumishi waliokuwepo hapa Shinyanga na Kahama ambao ni wanawake wameweza kufanya kazi zao kwa uweledi na umakini mkubwa na kuleta tija kwa jamii pamoja na wao wenyewe ambapo wapo waliopanda na kuwa Wakuu wa Mashtaka wa Mikoa na Wilaya  kwenye maeneo mbalimbali hivyo watumishi wapya wanapaswa kuiga mfano wa wengine.” Amesema Mkurugenzi Kweka”

Bw. Kweka amesema kuwa Ofisi ya  Mkoa wa Shinyanga imekuwa mfano katika utendaji kazi wake na kuamsha hali katika maeneo mengine ambapo amewataka waajiriwa wapya kuwa mabalozi wazuri wa kazi za Ofisi hiyo.

Akizungumza kwa niaba Kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Kahama Bw. Robert Kwela amewataka watumishi hao kuishi katika misingi ya ajira kwa kuwa ni wengi wanaotafuta, sambamba na kuwakata Vijana waliongia kazini katika ajira mpya kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa weledi na kutenda haki.

Naye Mkuu wa Mashtaka Mkoa wa Shinyanga Bi. Ajuaye Zegheli  amewahakikisha ushirikiano na  watumishi wapya sambamba na kuwataka wanaposhughulika na mashtaka kutanguliza maslahi mapana ya umma na si kutanguliza mahitaji yao binasfi.

Aidha watumishi hao pia wametoa azwadi mbalimbali ikiwemo tunzo za heshima kwa watumishi wenzao ikiwa nis ehemu ya kutambua mchango wako katika utumishi  wakati wakiwa Mkoani  Shinyanga.ambapo pia Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP) Sylvester Mwakitalu amepewa tunzo ya heshima kwa mchango wake katika usimamizi na usikilizaji wa changamoto za watumishi hao.

Tazama Picha mbalimabali katika matukio yaliyofanyika






















 

 

 

 

 

Share:

MKURUGENZI KWEKA AWATAKA WAENDESHA MASHTAKA NA WADAU KUHAKIKISHA HAKI ZA WATOTO ZINALINDWA

 Mkurugenzi wa Divisheni ya Utenganishaji wa Shughuli za Mashtaka na Upelelezi Bw. Tumaini Kweka amewataka Waendesha Mashtaka na Wadau kutoka Taasisi mbalimbali kuhakikisha wanatoa michango yao kwa usahihi katika kuboresha Rasimu ya Mwongozo wa Uendeshaji wa Kesi za Watoto kwa lengo la kulinda haki zao.

Mkurugenzi Kweka amebainisha hayo wakati akifungua Kikao kazi cha Wadau kwa ajili ya kutoa maoni ya kuboresha Rasimu ya Mwongozo wa Uendeshaji wa Kesi za Watoto kwa Waendesha Mashtaka kinachofanyika Jijini Dodoma kuanzia tarehe 20 hadi 21 Julai, 2023.

Aidha, Mkurugenzi Kweka ameeleza kuwa, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha wanawalinda na kuwajenga Watoto kuwa  raia bora hapo badae  hivyo Waendesha Mashtaka na Wadau wanapaswa kuboresha Rasimu ya Mwongozo wa Uendeshaji wa Kesi za Watoto  kulingana na mahitaji husika zikiwemo changamoto na mapungufu katika uendeshaji wa kesi hizo.



Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .