• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

"Mapambano dhidi ya Uhalifu tumeyapa kipaumbele" - DPP

 Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Sylvester Mwakitalu ametoa onyo kwa Watanzania ambao wanajihusisha na vitendo vya kiuhalifu na kuahidi kuongeza mikakati mipya ili kuhakikisha kwamba wanakabiliana na Uhalifu kwa nguvu zote ili wahalifu watambue kwamba uhalifu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haulipi.

Mkurugenzi Mwakitalu ameyasema hayo wakati akifungua Kikao cha Menejimenti, Wakuu wa Mashtaka, Wakuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mikoa na Wakuu wa Upelelezi Mikoa kinachofanyika tarehe 29 Septemba hadi 01 Octoba, 2023 Makao Makuu Jijini Dodoma.

Pia Mkurugenzi Mwakitalu ameeleza kuwa lengo kuu la kikao hicho ni kufanya tathmini ya utendaji kazi kwa kipindi cha mwaka mmoja kulingana na Maazimio waliyoyaweka na kuangalia ni kwa kiasi gani Maazimio hayo yametekelezeka, changamoto walizokutana nazo na sababu ya changamoto hizo, pamoja na kujadili kuweka malengo ya mwaka mwingine unaokuja.

Sambamba na hayo Mkurugenzi Mwakitalu ameeleza kuwa Makosa ya Rushwa, Uhujumu Uchumi na Ufisadi yana athari kubwa sana katika jamii kwani yanaongeza gharama za maisha na pia yanasababisha wananchi kukosa baadhi ya huduma ambazo wangeweza kuzipata. 

"Kusipokuwa na amani, kusipokuwa na utulivu hakuna mtu ambae atakwenda kufanya shughuli za maendeleo". Ameyasema hayo Mkurugenzi Mwakitalu.

Aidha, Mkurugenzi Mwakitalu ameendelea kueleza kuwa endapo Madawa ya Kulevya yataendelea kutumika pasipo kudhibitiwa basi nguvu kazi ya taifa itapotea.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Kamishna wa Polisi Salum Hamduni amesema kuwa moja ya jukumu walilonalo ni kuhakikisha wanaendelea kushirikiana na kufanya kazi kwa kwa pamoja kama timu  ili kusogeza huduma kwa wananchi hususani katika kuharakisha masuala ya uchunguzi wa uendeshaji wa mashtaka.

"Katika utekelezaji wa majukumu yetu tunagusa moja kwa moja haki za wananchi." Ameyasema hayo Mkurugenzi Mkuu Salum Hamduni.

Naye Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini  Kamishna wa Polisi Ramadhani Kingai ameeleza kuwa ushirikiano ni jambo muhimu sana katika kuwatendea haki wananchi kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



Share:

WAZIRI CHANA AZINDUA MIONGOZO MITATU (3) KUTOKA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA

 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amefanya Uzinduzi wa Miongozo Mitatu kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambayo ni Kuwajali na kuwalinda Mashahidi, Urejeshaji na Utaifishaji Mali zinazotokana na Uhalifu pamoja na Ushirikiano wa Kisheria katika Masuala ya Jinai. 



Uzinduzi huo umefanyika tarehe 27 Septemba, 2023 Jijini Dar es salaam ikiwa na lengo la kusaidia kuleta ufanisi na kuwezesha kujenga mfumo imara wa Kisheria katika upatikanaji wa Haki Jinai utakaowawezesha Wananchi kufanya shughuli zao kwa amani, utulivu na usawa.

Waziri Chana amesema kuwa Miongozo hii inatija kubwa kwa mashahidi ambao ndio nguzo muhimu katika upatikanaji wa Haki Jinai nchini kwani ili kuleta amani katika nchi na kutenda haki panahitajika kuwa na mashahidi.



Pia Dkt. Pindi Chana alitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuunda Tume ya kuangalia jinsi ya kuboresha Taasisi za Haki Jinai nchini kwani uamuzi huo unalenga kuhakikisha kuwa mapendekezo yaliyotolewa yatasaidia kuboresha mfumo wa Haki Jinai kwa kusaidia wananchi wengi kupata haki zao ikiwemo ulinzi wa mashahidi.



Aidha Waziri Chana ametoa wito kwa wananchi kuwa mabalozi wa amani kwa kutoa ushirikiano wa kutosha pale ambapo wanaona kuna uhalifu umefanyika au unafanyika wasiache kutoa taarifa katika vyombo husika.



"Ikiwa kama kuna eneo mtu kwa namna moja ama nyingine au kikundi cha watu watakuwa wanatenda uhalifu, sisi kama Wizara tutakuwa tayari kuwapokea kama wateja wetu halali. Tunahitaji Tanzania iwe ni mfano wa kuigwa na Mataifa mbalimbali kwani Tanzania sio sehemu salama ya Makosa ya Jinai." Ameyasema hayo Waziri Chana.



Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Sylvester Mwakitalu amesema kuwa wana imani Miongozo hiyo itaenda kuwaongezea tija katika utendaji wao wa kazi za kila siku.



Pia Mkurugenzi Mwakitalu alitoa shukrani kwa Wadau mbalimbali, Wasimamizi wa Sheria na Vyombo vya Uchunguzi kwa ushirikiano mkubwa walioutoa katika kuandaa nyaraka za Miongozo hiyo.



"Kwa kushirikiana na Taasisi hizi tumeweza kuelewa maeneo ambayo yana mapungufu katika utendaji kazi wetu kwa kufahamu changamoto pamoja na kuzitafutia ufumbuzi kwa kuweka katika Miongozo yetu." Ameyasema hayo Mkurugenzi Mwakitalu.



Sambamba na hilo Mkurugenzi Mwakitalu ameeleza kuwa kupitia miongozo hiyo itasaidia kuwa na usimamizi unaofanana katika kushughulikia Mashauri ya Jinai kutoka sehemu mbalimbali na pia itasaidia kuhakikisha wahalifu hawanufaiki na mali wanazopata kwa njia ya uhalifu, au mali zinazotumika katika kutenda uhalifu.



Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .