• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

"Niwapongeze watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa kazi nzuri mnayoifanya" NAIBU WAZIRI MHE. JUMANNE SAGINI

 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amewapongeza watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa kazi nzuri wanaiyofanya katika uendeshaji wa mashauri ya Jinai. 



"Mashauri tunayoshinda ni mengi kuliko tunayofeli kinyume na ilivyokuwa hapo awali. Kuwepo kwa ofisi hii imeonyesha tija iliyo bayana."

Naibu Waziri amebainisha hayo wakati alipotembelea Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma tarehe 04 Juni, 2024 na kuzungumza na Watumishi wa ofisi hiyo.

Sambamba na hilo Mhe. Naibu Waziri amewataka watumishi hao kuendelea kutekeleza majukumu yao ya kikatiba ili kuiwezesha nchi kwenda mbele na uhalifu uweze kupungua.

Pia Mhe. Jumanne ameagiza watumishi hao kuweka kipau mbele cha mafunzo ili kuweza kuwasaidia kuongeza ujuzi katika makosa ya jinai hususani katika masuala ya kiusalama ya kimtandao.

"Msisite kutoa elimu kwa wale ambao wanakwamisha kazi zenu. Wakati mnajenga uwezo wenu wale wadau wenu mnaoona wanahitaji kupata elimu ni vizuri mkajumuika nao ili kuimarisha umoja." Amebainisha hayo Mhe. Sagini.



Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .