• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

ACHENI KUFANYA SHUGHULI ZA KIBINADAMU KWENYE HIFADHI YA BONDE LA KILOMBERO TAFUTENI SEHEMU ZINGINE

 Mkurugenzi wa Mashtaka Bw.Biswalo Mganga akihutubia wageni walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Kilombero uliofanyika tarehe 15 Februari,2021

NA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA-MOROGORO.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw Biswalo Mganga amewataka Wananchi wanaofanya shughuli za kilimo katika maeneo ya hifadhi kusitisha shughuli hizo  na kwenda kutafuta sehemu nyingine za kuendeshea shughuli zao ili kulinda mazingira.

Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Kilombero alisema wakati wote maslahi ya Taifa yanatangulia maslahi binafsi hivyo ulinzi wa hifadhi ni jambo.muhimu katika kulinda maslahi mapana ya  Taifa.

Alisema bonde la Kilombero ni eneo linalotegemewa sana katika mradi wa Umeme wa Mwalimu Nyerere unaojengwa Rufiji Pwani hivyo uharibifu wa maliasili katika bonde hilo haukubaliki hata kidogo.

Alisema mpaka hivi sasa bado wapo watumishi wa Serikali wanaenda kulima na kufuga katika maeneo ya Bonde la mto Kilombero  ninawataka waache kufanya hivyo kwa kuwa wanaharibu mazingira.

"Sitaangalia sura ya mtu, awe mbunge,mwanasiasa, kiongozi wa dini katika kulinda bonde hili.nitachukua hatua kwakuwa maslahi binafsi hayawezi kuzidi maslahi ya Watanzania Milioni Sitini." Alisisitiza Mkurugenzi wa Mashtaka Mganga.

Alisema Serikali imewekeza fedha nyingi katika mradi wa Umeme wa Mwalimu Nyerere na Bwawa hilo kwa kiasi kikubwa linategemea maji kutoka Kilombero hivyo uharibifu ukitokea halafu maji yakikosekana   Taifa litakuwa limepoteza fedha nyingi, lakini tukizembea fedha za Taifa zitakuwa zimepotea. 

Aidha, alisema kuwa  muendelezo wa shughuli za kilimo kwenye maeneo hayo   husababisha nchi yetu itaendelea kuagiza umeme kutoka nje ya nchi, viwanda vyetu vitaendelea kukosa umeme wa uhakika.

Nikiwa mimi DPP  sitaangalia sura ya mtu, Maslahi ya Mbunge au diwani tunaweka pembeni wakati wote tunatanguliza maslahi ya Taifa kwa kuwa hatuwezi kuona mradi wa umeme wa Mwalimu Nyerere unaharibika kwa sababu ya maslahi ya watu wachache.

Niwaombe  Wakuu wa Wilaya msirudi nyuma kuhakikisha mnazuia shughuli za kibinadamu katika eneo hilo  na kuhakikisha  Sheria zibafuatwa, pia wananchi wahakikishe wanatafuta maeneo mengine ya kulima. Alisisitiza Mkurugenzi wa Mashtaka.

Mkurugenzi wa  Mashtaka nchini DPP Biswalo Mganga akiwa pamoja na wakuu wa Wilaya za Kilombero Mhe.Ismail Mlawa  na Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Stephano Kaliwa wakielekea eneo la tukio kwa ajili ya ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilayani Kilombero.
Viongozi wa dini mbalimbali, watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero na wananchi wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mashtaka (hayupo pichani) wakati akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Kilombero iliyofanyika mjini Ifakara  tarehe 15 Februari, 2021.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya  Mashtaka Mkoani Morogoro wakiwa wameketi kwa pamoja wakiendelea kufautilia hotuba za viongozi wa wilaya.
Viongozi mbalimbali wakiwepo Wakuu wa Wilaya na Viongozi wa dini wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Biswalo Mganga wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Kilombero uliofanyika  tarehe 15 Februari,2021.
Mkurugenzi wa Raslimali Watu na Utawala Bw. Seushi Mburi akitoa neno la shukrani wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilayani Kilombero uliofanyika  tarehe 15 Februari,2021
Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe.Ismail Mlawa akihutubia katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Kilombero uliofanyika  tarehe 15 Februari,2021 mjini Ifakara


Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Mhe. Stephano Kaliwa akihutubia katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Kilombero uliofanyika tarehe 15 Februari,2021 mjini Ifakara.

Share:

JIEPUSHENI NA VITENDO VYA RUSHWA HAKIKA SITAMVUMILIA MTUMISHI ATAKAYEHUSIKA NA RUSHWA AMESEMA DPP BISWALO MGANGA

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw.Biswalo Mganga akizungumza na washiriki wa mafunzo ya Ukusanyaji, Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa njia ya  Kidijitali kutoka Mikoa 26 ya Tanzania Bara.
SINGIDA.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw.Biswalo Mganga amewataka  Makatibu Sheria nchini  kuhakikisha wanatumia vizuri mfumo mpya wa Ukusanyaji, Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa njia ya  Kidijitali hali itakayowezesha utoaji wa Takwimu sahihi kwa maendeleo ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi  wa Mashtaka Bw. Biswalo Mganga  wakati akifunga Mafunzo ya siku 6 ya Makatibu Sheria kutoka Mikoa yote ya Tanzania bara mafunzo yaliyofanyika Manispaa ya Singida yakiwa  na lengo la kuwajengea uwezo makatibu hao katika  Ukusanyaji, Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa mfumo wa Kidijitali.

Ameeleza kuwa jukumu la watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ni kuwajibika kwa umma  na serikali hivyo Makatibu  Sheria wanalo jukumu kubwa la kuhakakikisha huduma bora za mashtaka zinawafikia wananchi na kuiona ofisi kuwa yao.

Naomba niseme jukumu kubwa tulilonalo ni kuwajibika kwa Umma, Taasisi na Serikali kwa kuhakikisha tunatoa huduma bora na za  kuvutia kwa wananchi,  nisingependa kusikia lugha mbaya toka kwenu zikiwahusu watu wanaokuja kwenu kutafuta msaada badala yake tumieni lugha nzuri kwani majalada yote yanapitia kwenu”amesema Bw.Biswalo 

Biswalo amesema Makatibu Sheria ndiyo mlango wa Kupokea majalada hivyo wasiwe chanzo cha kujihusisha na vitendo vya rushwa kwani kufanya hivyo kunadhoofisha maendeleo ya Nchi na Taifa kwa ujuma

Sitaki kusikia ninyi  Makatibu  Sheria mnakuwa vyanzo vya kujihusisha na vitendo vya Rushwa ndani ya taasisi kwa sababu tu watu wote wanaanzia kwenu  na wala msidanganyike kwani mkifanya hivyo mtaishia  pabaya, siko tayari kumvumilia mtu anayekula RushwaBw.Biswalo

Katika hatua nyingine Mkurugenzi Biswalo amewaasa watumishi hao kutoharibu taaluma yao ya Ukatibu Sheria  kwa kujihusisha na uvujishaji wa siri za Nyaraka za Ofisi kwani kufanya hivyo ni kinyume cha maadili pia hali ambayo inahatarisha usalama wa nchi.

Niwaombe ninyi Makatibu Sheria mnayo nafasi kubwa ya kutupatia na kusaidia  taarifa za siri juu ya watu wanaofutilia majalada yetu hususani makanjanja ili tumfahamu mtu anayefuatilia ana lengo gani na tujue tunaanzia wapi kumchukulia hatuaBw.Biswalo

Aidha, Biswalo akizugumzia suala la Mfumo mpya wa Ukusanyaji,Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa mfumo wa Kidijitali amewataka kuhakikisha taarifa zinaingizwa kwenye mfumo kwa uhakika na umakini huku akiwaonya Makatibu hao kwenda kufanya kazi zao kwenye internet Café ambako nyaraka za serikali husalia  na kuhataraisha usalama wa ofisi na nchi kwani watu wabaya wanaweza kuzitumia kwa maslahai yao binafsi.

Ni marufuku kutumia barua pepe  za Ofisi kwenye Kompyuta za internet  café utumike ndani ya ofisi na Kompyuta za ofisi tu kwani kutumia huko taarifa zinabaki  na watu wanaanza kudukua hivyo kwa hili atakayebainika sitamwonea huruma lazima hatua kali zichukulie dhidi yakeBw.Biswalo

Biswalo ameongeza kuwa utumiaji wa mfumo huo mpya wa Uchakati na utumaji wa taarifa  isiwe sababu ya kuachana na mfumo wa zamani wa regista  ambapo amesisitiza mifumo yote kwenda samabmba hadi pale mfumo wa kidijitali utakapokuwa umeimarika na kusimama vizuri

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Kesi na Uratibu wa Upelelezi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  ambaye anashughulikia Usimamizi wa Kesi  Bw. Tumaini Kweka amesema kuwa  Makatibu Sheria ni watu muhimu sana hivyo mafunzo hayo yamejikita kuwajengea uwezo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa viwango vinavyotarajiwa pamoja na kuwawezesha kukabiliana na changamoto wanazokutana  nazo

Naomba  kukutaarifu kuwa mafunzo haya yameshirikisha washiriki 30 kutoka Mikoa yote 26 ya Tanzania Bara  hivyo tuna imani kuwa kile walichojifunza hapa kinaenda kuwa chachu kubwa kwa wengine waliosalia kwenye maeneo yao”amesema Bw. Kweka 

Kweka ameongeza kuwa katika mafunzo hayo jumla ya Mada nane zimewailishwa kutoka kwa watalaamu wa ndani na nje ya taasisi hiyo waliowasilisha mada kwa kina na washiriki kupata nafasi ya kuuliza maswali na kujibiwa”

Naye mwakilishi wa washiriki wa Mafunzo hayo ya Ukusanyaji,Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa njia ya  Kidijitali Bi Faraja amesema kuwa mafunzo hayo kwao ni chachu kubwa ya kuboresha  utendaji kazi wao hususani kuendana  na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Mafunzo  hayo  yameandaliwa kwa ushirikiano wa  Idara  ya  Usimamizi wa Kesi  na uratibu wa upelelezi na Programu ya BSAAT kupitia Divisheni ya Makosa ya Udanganyifu, Utakatishaji fedha na Rushwa Ofisi ya Taifa  ya Mashtaka.  Idrisa Heri Swalehe Afisa Tehama, kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka(NPS) Mkoani Mwanza  akitoa elimu ya Ukusanyaji,Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa mfumo wa KidijitaliWashiriki wakiendelea kujifunza kwa vitendo wakati wa mafunzo ya  Ukusanyaji, Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa njia ya  Kidijitali kutoka Mikoa 26 ya Tanzania Bara.Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Biswalo Mganga akitazama namna  zoezi la elimu kwa vitendo linavyofanyika baada ya Makatibu Sheria  kupata Mafunzo  ya Ukusanyaji, Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa kwa mfumo wa  Kidijitali.Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Kesi na Uratibu wa Upelelezi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  ambaye anashughulikia usimamizi wa Kesi Tumaini Kweka akifuatilia kwa ukaribu mafunzo.Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Biswalo Mganga akiwa ameketi kwa pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Kesi na Uratibu wa Upelelezi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  ambaye anashughulikia usimamizi wa Kesi Tumaini Kweka wakiendelea kufuatilia mafunzo.

Bi Faraja mwakilishi wa washiriki wa Mafunzo hayo ya Ukusanyaji,Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa  kwa njia ya  Kidijitali akishukuru kwa niaba ya washiriki wenzake.
Baadhi ya  washiriki wakiedelea kujifunza kwa vitendo namna ya kutumia mfumo mpya wa kidijitali  wa Ukusanyaji, Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai, na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa.
Share:

HAKIKISHENI MNAZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WENU KWENYE MAENEO YENU YA KAZI BW.MAKALLO NAIBU DPP

Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Edson Makallo akifungua mafunzo ya Ukusanyaji, Uchakataji, Utumaji na Utunzaji wa Takwimu  za Kesi za Jinai na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa kwa Makatibu Sheria yanayofanyika mkoani Singida kuanzia tarehe 3 Februari,2021 hadi tarehe 08 Febry,2021. Kushoto kwa Bw. Makallo ni  Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Uratibu wa Upelelezi Bi. Neema Mwanda.

NA MWADISHI Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Edson Makallo akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya Ukusanyaji, Uchakataji,Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa kwa Makatibu Sheria yanayofanyika Mkoani Singida kuanzia leo tarehe 3 Februari 2021 hadi 08 Februari,2021. Kushoto ni Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa Ofisi ya  Taifa ya Mashtaka Bw. Sheusi Mburi pamoja na viongozi wengine kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Edson Makallo  amewasihi watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuzingatia Maadili katika maeneo yao ya kazi pamoja na kufanya kazi kwa bidii.

Naibu Mkurugenzi Makallo ameyasema hayo mapema leo wakati akifungua mafunzo ya ukusanyaji, uchakataji, utumiaji na utunzaji wa takwimu za kesi za Jinai na kumbukumbu  za makosa ya Rushwa kwa Makatibu Sheria wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka yanayofanyika Mkoani Singida kuanzia tarehe 03 Februari 2021.hadi tarehe 08  Februari,2021

Bw. Makallo amesema kada ya utumishi wa Makatibu wa  Sheria inakumbana na changamoto mbalimbali za kiutendaji na kimaadili  hivyo mafunzo hayo wanayopatiwa yatumike kuwasaidia na kuboresha utendaji wao wa kazi.

Amesema katika miaka ya karibuni dunia imeshuhudia kuwepo kwa mabadiliko makubwa katika nyanja mbalimbali za maisha ya mwanadamu kiuchumi,kijamii, kisiasa, kiteknolojia na kiutamaduni ambapo athari za mabadiliko  hayo ni pamoja na kubadilika kwa mbinu za kupanga na kutekeleza uhalifu na hivyo kuwataka Makatibu wa Sheria wakiwa ni miongoni mwa watoa huduma katika taasisi ya Haki Jinai kukumbuka kuwa wana jukumu kubwa la kuhakikisha wanashiriki katika kupambana na kuzuia uhalifu huo kwa njia ya kutekeleza vema majukumu yao.

Aidha, amesema kuwa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imejipanga vyema katika kushughulikia matendo ya mmomonyoko wa maadili kwa watumishi wa Umma ambapo hatua madhubuti zimekuwa zikichukuliwa kwa watumishi wanaobainika kujihusisha na vitendo vya utovu wa nidhamu.

Amesema watumishi wa Umma wakizingatia miiko iliyopo katika utendaji wao wa kila siku huleta matokeo chanya kwa huduma wanazotoa kwa jamii na hivyo jamiu hujenga imani kwa serikali na kuleta hali ya Usalama.

Bw. Makallo alitoa rai kwa Makatibu Sheria waliohudhuria mafunzo hayo  kuwa kila aliyepata mafunzo arudipo katika sehemu yake ya kazi  kuweka ujuzi aliopata kwa vitendo na kushirikisha ujuzi walioupata kwa wengine  ambao hawajapata nafasi ya kuhudhuria mafunzo ili kupanua ushiriki wa mafunzo wa Makatibu Sheria wengi zaidi.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kutunza siri zinazohusu taarifa za majalada yanayowafikia  huku wakielewa kwamba suala la utunzaji wa siri ni la lazima kwa watumishi wote wa Umma.

Mafunzo hayo ya siku sita kwa Makatibu Sheria  yameandaliwa kwa ushirikiano wa Divisheni ya Usimamizi wa Kesi na Uratibu wa Upelelezi  na  Divisheni ya Makosa ya Udanganyifu, Utakatishaji Fedha na Rushwa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Katika mafunzo hayo mada mbalimbali  zitatolewa zikiwepo mada juu ya Maadili ya Makatibu Sheria, Kutunza na kushughulikia  majalada ya rushwa, ukusanyaji, uchakataji na utumaji wa takwimu za kesi, utunzaji na mfumo wa regista ya ofisi,mfumo wa kielektroniki wa upokeaji na utunzaji wa majalada, utunzaji wa kumbukumbu na  nyaraka za serikali pamoja na.masuala mengine yanayohusu maadili.

Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya  Usimamizi wa Kesi za Jinai   Bw. Tumaini Kweka akizungumza  katika mafunzo ya ukusanyaji, uchakataji na utumiaji wa takwimu na kumbukumbu za makosa ya rushwa kwa Makatibu Sheria yanayofanyika Mkoa wa Singida kuanzia leo tarehe 3 Februari, 2021 na kumalizika tarehe 08 Februari,2021.Katibu Sheria Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Gilley Manara akitoa taarifa ya majukumu ya kiofisi katika mafunzo ya ukusanyaji, uchakataji na utumiaji wa takwimu na kumbukumbu za makosa ya rushwa yanayofanyika Mkoani Singida kuanzia tarehe 3 Februari, 2021 na kumalizika tarehe 8 Februari, 2021.

Mkurugenzi Rasilimali Watu Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Seushi Mburi akitoa mada juu ya maadili ya utendaji kazi katika utumishi wa umma na mfumo wa kazi wa mapitio na tathmini ya utendaji kazi  kwa Makatibu Sheria ambao wameudhuria mafunzo ya ukusanyaji, uchakataji na utumiaji wa takwimu na kumbukumbu za makosa ya rushwa yanayofanyika Mkoani Singida kuanzia tarehe 3 Februari, 2021 na kumalizika tarehe 8 Februari, 2021.
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Edson Makallo akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya Ukusanyaji, Uchakataji,Utumaji na Utunzaji wa Takwimu za Kesi za Jinai na Kumbukumbu za Makosa ya Rushwa kwa Makatibu Sheria yanayofanyika mkoani Singida kuanzia tarehe 3 Februari 2021 hadi 08 Februari,2021. Kushoto kwa Bw. Makallo.ni Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa Ofisi ya  Taifa ya Mashtaka Been. Sheusi Mburi pamoja na viongozi wengine kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .