Mwonekano wa Mbele wa Jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam -
Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti
Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.
-
UKATAJI WA UTEPE
UKATAJI
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.
-
WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMDANGANYA DPP KUWA NI MAOFISA USALAMA WA TAIFA
Mwonekano wa Mbele wa Jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam DPP MWAKITALU ASEMA ATAPELEKA MAHAKAMANI MASHAURI YENYE USHAHIDI KAMILI.
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu akipokea Maelezo kutoka kwa Mkuu wa Gereza la Mahabusu Segerea Mrakibu Mwandamizi wa Magereza(SSP)Daniel Mwakyoma wakati alipotembelea Gereza hilo Juni 13,2021.
Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP)
Sylvester Mwakitalu amehitimisha ziara yake ya kutembelea na kukagua hali ya Magereza ya Mkoa wa Dar es Salaam baada ya kutembelea na kuzungumza
na Mahabusu pamoja na wafungwa walioko katika magereza yote matatu ya mkoa huo.
Akizungumza mara baada ya
kujionea hali ilivyo katika Magereza hayo, baada ya kuhitimisha ziara kwa kutembelea
Gereza la Mahabusu Segerea DPP Mwakitalu
amesema Changamoto alizoziona ndani ya
magereza hayo zitamsadia katika kufanya maamuzi na kuboreha utendaji kazi wa
Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.
DPP Mwakitalu alisema
changamoto zilizowasilishwa na baadhi ya mahabusu walioko gereza la Segerea
ambazo hazipo ndani ya uwezo wa Ofisi ya
Mashtaka atakahikikisha anazifikisha kwa wahusika ili ziweze kutafutiwa
ufumbuzi ambapo amesema maeneo yanayohitaji suluhisho la pamoja atahakikisha
anakaa na wadau ili kutafuta suluhisho la pamoja.
“Kwa changamoto ambazo ziko
chini ya ofisi yangu, nitazifanyia kazi kwa
haraka kadri iwezekanavyo ili haki
iweze kutendeka,haya mengine
ambayo yako nje ya Ofisi yangu nitawashirikisha wadau wakiwemo mahakama,
wapelelezi na wachunguzi ili tuwe na suluhu ya pamoja”Alisema DPP Mwakitalu
Aidha, DPP Mwakitalu akizugumzia
chagamoto ya kuchelewa kwa upelelezi wa mashauri mbalimbali alisema kuwa wapelelezi
wanaoshugulikia kesi ni wadau wake wa karibu
kwani bila uwepo wao yeye hawezi kufanya kazi hivyo ameahidi kukaa kwa
pamoja ili kesi zilizoko mahakamani ambazo
upelelezi wake haujakamalika uweze kufika mwisho.
Alisema Ofisi ya Taifa ya Mashtaka katika kutekeleza
majukumu yake itaendelea kufanya kazi zake kwa kutenda haki.
Mwakitalu alisema kuwa kwa sasa Ofisi yake kwa pamoja na watendaji
wataanza kazi ya kupitia upya majalada ya kesi ili kubaini kama yana ushahidi
wa kutosha kesi ziendelee na kama ushahidi wake ni hafifu atayafanyia maamuzi.
“Naomba niwaeleze
changamoto hizi na ushauri wenu nimeupokea kwa sasa hatua tulizonazo ni kupitia upya majalada ya kesi
ili kuona lipi linafaa kuendlea a lipi linafaa kufanyiwa maamuzi upya”alisema
DPP Mwakitalu
Katika hatua nyingine DPP alisema kuwa Ofisi yake kwa
sasa itahikikisha inapeleka kesi
mahakamani zenye ushahidi kamili na zile ambazo bado hazijapata Ushaihidi
kamili hazitafikishwa Mahakamani ili kuondoa changamoto ya Msongamano Magerezani .
Kuhusiana na suala la utoaji wa vibali vya kesi DPP
Mwakitalu alisema kuwa atahakikisha vibali vya Kesi(Concert) ambazo zimekwama kutokana na kukosa kibali
hicho atahakikisha vibali hivyo
vinatolewa ili kesi ziweze kuendelea.
Aidha, DPP Mwakitalu ametembelea magareza ya Keko,Segerea
na Gereza Kuu Ukonga ambapo alisema kuwa huo ni Mwendelezo wa ziara zake za
kutembelea na kukagua hali ya magereza hapa nchini, kusikiliza kero na changamoto za wafungwa na mahabusu ili
Ofisi yake iweze kuzitafutia Suluhu
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu akiwasili katika gereza la Mahabusu Segerea na kupokelewa na mkuu wa gereza hilo Mrakibu Mwandamizi wa Magereza Daniel Mwakyoma Mapema juni 13,2021.
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu(Kushoto)akisalimiana na Mkuu wa Gereza la Mahabusu wanawake Segerea Mrakibu wa Magereza Iyunge Saganda (wa pili kutoka kushoto) wakati wa ziara ya kutembelea na kusikiliza changamoto za Mahabusu .
Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu akisalimiana na baadhi ya maafisa wa magereza katika gereza la Mahabusu Segerea Mkoani Dar es salaam wakati wa ziara yake.Mkuu wa Gereza la Mahabusu Segerea Mrakibu Mwandamizi wa Magereza(SSP)Daniel Mwakyoma akiwaongoza Viongozi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)Sylvester Mwakitalu kuelekea Gereza la Mahabusu wanaume.
DPP MWAKITALU ATEMBELEA NA KUKAGUA HALI YA MAGEREZA UKONGA NA KEKO JIJINI DAR ES SALAAM, AAHIDI KUZITAFUTIA UFUMBUZI CHANGAMOTO
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Sylvester Mwakitalu amefanya ziara ya ukaguzi katika Magereza ya Keko na Gereza Kuu Ukonga ya jijini Dar es Salaam ili kujionea hali halisi ya magereza hayo, kuzugumza na mahabusu pamoja na wafungwa na kuahidi kushirikiana na vyombo vingine kutatua changamoto zinapelekea kuwepo kwa msongamano ndani ya magereza hayo.
Akizungumza mara baada ya kuhitimisha ziara hiyo aliyoongozana na baadhi ya watendaji kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu na Mkoa wa Dar es Salaam , Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Mwakitalu amesema lengo la ziara hiyo ni kujionea hali halisi ya magereza, kuwasikiliza mahabusu na wafungwa ili kubaini changamoto mbalimbali zinazowakabili mahabusu na wafungwa kufuatia kesi mbalimbali zilizoko mahakamani.
“Ujio wangu hapa ni kwa ajili ya kujionea hali halisi ya msongamano pamoja na kusikiliza kero za mahabasu,
wafungwa na magereza kwa ujumla ili niweze kufanyia kazi maeneo yale yanayohusu ofisi yangu “Alisema
DPP Mwakitalu.
Mkurugenzi Mwakitalu amesema Magereza mengi nchini
yanakabiliwa na msongamano mkubwa wa wafungwa
na mahabusu kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuongezeka kwa hali ya uhalifu nchini.
Aidha, Mkurugenzi Mwakitalu amewataka watanzania kuacha
kujihusisha na uhalifu hali ambayo inachangia kuongezeka kwa msongamano
magerezani huku akiahidi kufanya kazi kwa nguvu na bidii ili mashauri yaweze
kusikilizwa kwa haraka na wakati.
Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Mashtaka ametembelea na
kujionea uzalishaji mkubwa wa Bidhaa (Fanicha) zinazotengenezwa na
wafungwa katika gereza kuu Ukonga
Ziara hiyo ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini imelenga katika kusikiliza, kupokea malalamiko na changamoto mbalimbali
zinazohusiana na masuala ya mashtaka ili ofisi yake iweze kuyatafutia ufumbuzi ili kupunguza changamoto na msongamano magerezani.
Katika ziara hiyo Mkurugenzi wa Mashtaka ameambatana na Mkurugenzi wa Divisheni ya Utenganishaji
wa Shughuli za Mashtaka na Upelelezi Bw. Oswald Tibabyekomya, Mkuu wa Mashtaka Mkoa
wa Dar es Salaam Bi. Mkunde Mshanga na Wakuu
wa Mashtaka Wilaya zote za Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini Bw. Sylvester Mwakitalu akiwa ameambatana na Viongozi wengine wakati wa zoezi la kutembelea magereza ya Ukonga na Keko Jijini Dar es Salaam mapema leo Juni 12,2021.


DPP MWAKITALU ATETA NA WATENDAJI WA MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI KISUTU AAHIDI USHIRIKIANO ILI KUMALIZA MRUNDIKANO WA MASHAURI.
Na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka --DSM.
Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini Bw. Sylvester Mwakitalu amekutana na kufanya mazungumzo na Watendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, mapema leo ikiwa ni sehemu ya kukuza Uhusiano na Ushirikiano katika utendaji, ili kuwezesha kumalizika kwa mrundikano wa Mashauri yaliyoko katika Mahakama hiyo.
Akizungumza na Mahakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,
Mkurugenzi wa Mashataka Bw. Mwakitalu amesema kuwa ili kesi ziweze kwenda kwa
kasi na usikilizwaji ufanyike kwa haraka, ni lazima Taasisi hizo zishirikiane
kwa ukaribu hali itakayosaidia kuondoa kero na changamoto zinazosababisha
kuchelewa kesi.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Mwakitalu amesema kuwa changamoto
ya Maridhiano(Pre Bargaining) ambayo imeonekana kuwa tatizo amehaidi ndani ya
wiki moja itashughulikiwa na kufanyiwa kazi ili ufanisi wa kazi uweze kuendelea,ambapo
timu ya maalumu ya Serikali ya mauala ya Kisheria itakutana na kuona namna ya kuboresha Sheria ya Maridhiano
katika Kesi mbalimbali hususani za Uhujumu Uchumi .
Kuhusiana na suala la Mashauri ambayo awali yalikuwa yana
Mkurugenzi, kutoa kibali cha kuendesha kesi, ili hali anaweza kuwakasimisha Utoaji
wa vibali hivyo Waendehsa Mashtaka wa Mikoa, Bw. Mwakitalu amesema kuwa yapo
Mashauri ambayo kwa mujibu wa Sheria
anaweza kuwaelekeza Waendesha Mashtaka wa Mikoa kuyashughulia, lakini yapo
mengine ambayo yanahitaji kibali chake.
“Kwa sasa Mashauri yote yatakayofikishwa Mahakamani ni yale
tu ambayo upelelezi wake umekamilika ikiwa ni mkakaki wa Mahakama ya Tanzania kupitia
kwa Jiji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Profesa Ibrahim Juma wa kutakwa Mashauri
yasizidishe Mwaka yakiwa hayajasikiizwa”Alisema Bw.Mwakitalu
Aidha Bw. Mwakitalu amesema kuwa kwa sasa atahakikisha
anasaini Kesi zote zinazo hitaji kibali chake ili zianze kusikilizwa katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili kuondoa mrundikano wa Mashauri hayo
Mahakamani.
Bw. Mwakitalu Ameongeza kwa kusema kuwa Kesi inapochukua muda mrefu upelekea
Mashahidi wengi kupotea na wengine kutoonekana kutokana na sababu mbalimbali
ikiwemo Kuhama au Vifo, ambapo amewahakikishia watendaji wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu, Ushirikiano mkubwa ili kuwezesha ufanikishaji wa Kesi na
kupunguza Mlundikano wake Katika Mahakama hiyo.
“Mfano mpaka sasa jumla ya Kesi 369 zimekwisha pitisha muda
wake hali inayochangia uwepo wa Malalamiko
ya Wananchi, hivyo basi mimi niwahakikishie Ofisi yangu na Watendeji wangu
hawatakuwa kikwazo kwa hili nikiwa DPP wakati wangu” Alisema Mkurugenzi wa
Mashtaka Bw. Mwakitalu.
Awali akisoma Risala kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)
Sylvester Mwakitalu, Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu Gedfrey Isaya amesema kuwa mkoa wa Dar es salaam unazo Mahakama za
Hakimu Mkazi Nne ambazo ni Hakimu Mkazi Kisutu,Mahakama ya Watoto,Hakimu Mkazi
Kivukoni/Kinondoni na Mahakama ya Jiji/Sokoine.
Hakimu Mkazi Isaya amesema kuwa kwa kipindi cha Januari
2021 hadi Juni 10,2021 Mashauri mbalimbali yameshughulikiwa ambapo Kesi 579
zilibaki kwa Mwaka 2020 huku Kesi 132 zikipokelewa hadi Mei, Kesi 167
zikisikiliszwa
Aidha Hakimu Isaya amesema kuwa zipo jumla ya Kesi 8 ambazo
zimechukua muda mrefu kutokana na Mashahidi kuwa changamoto katika upatikanaji
wake hali ambayo inapelekea Kesi hizo kuchukua muda mrefu pasipo kusikilizwa.
Hakimu Mkazi Isaya ameongeza kwa kusema kuwa wanakabiliwa
na changamoto kubwa moja ni Upelelezi wa Mashauri kuchukua muda mrefu hata kwa
Mashauri ya bhangi na kuchangia Mlundikano wa Kesi, pili Mashauri mengi kuwa ya
muda mrefu hii ikisababishwa na kutopatikana kwa Mashahidi, Mashauri mengi kusubiri Kibali cha Mkurugenzi
wa Mashataka na hivyo mengi yanachelewa hata kabla ya kibali kutolewa.
Hakimu Mkazi Isaya maehitimisha kwa kusema kuwa Mashauri
mengi ya Nyara za Serikali,Madawa ya kulevya na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA)huchukua muda mrefu sana katika
upelelezi wake.
Kikao hicho kilichofanyika leo Juni 11, ni Mwendelezo wa kikao cha awali ambacho kilifanyika mwezi Mei Tarehe 21, mwaka huu kati ya Mkurugenzi wa Mashtaka na Watendaji na watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kikiwa na lengo la kutatua changamoto na malalamiko ya Mlundikano wa Kesi katika Mahakama hiyo.
Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Mashtaka ametembelea gereza la Keko jijini Dar es Salaam kujionea hali halisi ya gereza hilo na kuzungumza na wafungwa pamoja na mahabusu wa gereza hilo.
Akizungumza katika gereza hilo Mkurugenzi wa Mashtaka alisema hali ya mrundikano wa mahabusu na wafungwa katika gereza hilo inampa hamasa ya kufanya kazi kwa nguvu, bidii na maarifa ili kutatua changamoto za Msongamano magereza
Bw. Sylvester amesema kuwa changamoto ya kuchelewa kwa upelelezi iliyowasilishwa kupitia risala iliyotolewa na mahabusu na wafungwa wa gereza hilo, Mkurugenzi wa Mashtaka alisema atakaa na wapelelezi ili kutatua changamoto hiyo na kufanya maamuzi yatakayosaidia kuondoa changamoto hiyo.
Aidha, Mkurugenzi wa Mashtaka aliahidi kwenda kuangalia upya hati za dhamana zilizotolewa ili kuona kama sababu zilizopelekea kutolewa kwa dhamana hizo zipo au hazipo na endapo zitakuwa hazipo kwa sasa ataziondoa.
Mkurugenzi
wa Mashtaka Nchini Bw. Sylvester Mwakitalu akizungumza na Wafanyakazi na Watendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam(hawapo Pichani) ikiwa ni mojawapo ya Mkakati wa Ofisi yake kuhakikisha Mashauri yanaendeshwa kwa weledi na kwa wakati.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylivester Mwakitalu akizungumza na watendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam kujadili namna Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam wanavyoweza kushirikiana kuondoa mashauri yaliyochukua muda mrefu yaliyokaa kwa muda mrefu katika mahakama hiyo. Jumla ya mashauri 369 bado hayajafanyiwa kazi ambapo kufuatia kikao hicho maamuzi ya kumaliza changamoto hiyo yamefikiwa Kulia kwake ni Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Mhe. Godfrey Isaya.





