• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

DPP AWATAKA MAKATIBU SHERIA KUFUATA MAADILI YA KAZI.

 



Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu amewataka Makatibu Sheria kufanya kazi zao kwa kuzingatia miiko na misingi ya utumishi wa umma.


Mkurugenzi Mwakitalu ameyasema hayo wakati akifungua kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu Sheria kutoka Mikoa na Wilaya mbalimbali nchini kilichoanza leo tarehe 17 hadi 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.


Bw. Mwakitalu aliendelea kuwaasa Makatibu Sheria kuwa baada ya kumaliza kikao kazi hiki wanapaswa kubadilika na kwenda kufanya kazi zao kwa uadilifu, na kwa moyo wa kujituma.


"Tumekabidhiwa dhamana Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, tucheze kama timu moja, tufanye kazi kwa kushirikiana ili kwa pamoja tusimame na tusonge mbele. Pamoja na changamoto mbalimbali tulizonazo lakini tujitahidi kufanya kazi kwa bidii." Amezungumza hayo Mkurugenzi wa Mashtaka nchini.

Nae pia Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka ambae pia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji wa Kesi Bi. Neema Mwanda alieleza kuwa lengo kuu la kikao kazi hiki ni kujifunza na kuongeza uelewa zaidi juu ya masuala mbalimbali ya kiutendaji katika kazi zinazofanywa na Makatibu Sheria, hivyo basi kupitia kikao kazi hiki ana mategemeo ya kuwa washiriki wote watatoka wakiwa wameongeza uelewa zaidi katika kazi zao tofauti na walivyokuja.

Share:

DPP AWATAKA MAKATIBU SHERIA KUFUATA MAADILI YA KAZI

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akitoa neno la ufunguzi wa kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu sheria kilichoanza leo tarehe 17 Disemba, 2021 hadi tarehe 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.

Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka ambae pia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji wa Kesi Bi. Neema Mwanda akitoa neno la kumkaribisha mgeni rasmi Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu kwa lengo la kufungua  kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu Sheria kilichoanza leo tarehe 17 Disemba, 2021 hadi tarehe 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Bw. Titus Mkapa akielezea malengo ya kukutana katika kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu sheria kilichoanza leo tarehe 17 Disemba, 2021 hadi tarehe 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.






katika kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu sheria kilichoanza leo tarehe 17 Disemba, 2021 hadi tarehe 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.



Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu Sheria wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu (hayupo pichani)  wakati akihutubia katika kikao hicho kilichoanza leo tarehe 17 hadi 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Jijini Dodoma.


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya  Mipango Bw. Mussa Magunguli akiwasilisha mada juu ya Mipango, Bajeti na Taarifa za Utekelezaji katika kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu sheria kilichoanza leo tarehe 17 Disemba, 2021 hadi tarehe 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala Bw. Leonard Mehta akitoa mada juu ya Wasilisho la Rasimu ya Mapendekezo ya Miundo ya Kiutumishi ya Makatibu Sheria katika kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu Sheria kilichoanza leo tarehe 17 Disemba, 2021 hadi tarehe 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.













Picha ya pamoja ikijumuisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu (katikati), Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Bw. Titus Mkapa (kulia), Kaimu Naibu Mkurugenzi ambae pia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji wa Kesi Bi. Neema Mwanda wakiwa na Makatibu Sheria kutoka Mikoa na Wilaya mbalimbali  walioshiriki katika kikao kazi cha Mkurugenzi wa Mashtaka na Makatibu sheria kilichoanza leo tarehe 17 Disemba, 2021 hadi tarehe 18 Disemba, 2021 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.








Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .