• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

NAIBU KATIBU MKUU AZINDUA TAARIFA YA UKAGUZI WA VIZUIZI WANAKOSHIKILIWA WATOTO WALIOKINZANA NA SHERIA.

 Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Khatibu Kazungu amefanya uzinduzi wa Taarifa ya Ukaguzi wa Vizuizi wanakoshikiliwa Watoto waliokinzana na Sheria ambao umefanyika tarehe 18 Julai, 2022 Jijini Dodoma.

                                                    


Katika hafla ya uzinduzi huo Dkt. Khatibu ameeleza kuwa mtoto ndio taifa la leo hivyo wasipowekeza kwenye maeneo ya watoto katika kiafya, kielimu na kiakili zaidi basi taifa hili litaangamia zaidi.

"Uwekezaji katika maeneo haya ni muhimu sana kwa watoto wetu, na ni moja ya sababu ambazo zinapelekea watoto hawa 435 kukutwa katika maeneo mbalimbali ya vizuizi hapa Tanzania. Hivyo juhudi zozote zinazolenga kuhusu ustawi wa watoto hazina budi kupongezwa." Amezungumza hayo Dkt. Kazungu

Aidha Naibu Katibu Mkuu alitoa pongezi kwa niaba ya Wizara ya Katiba na Sheria kuipongeza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa kuona umuhimu wa kukagua vizuizi hivyo kwa lengo la kulinda watoto walio kwenye mkinzano wa vyombo vya sheria. Pia alitoa pongezi kwa wadau wote  walioshirikiana na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka katika kukamilisha zoezi hilo kwa mafanikio makubwa                                               

Pia Dkt. Kazungu aliendelea kueleza kuwa matokeo yaliyofanyika ya ukaguzi huo ni vema yatumike kama kizio cha kaguzi zitakazoendelea ili kuweza kuona kama wanasonga mbele ama hawajaweza kuimarisha haki za watoto.

"Natambua jukumu la haki jinai sio la Wizara ya Katiba na Sheria peke yake, hivyo ni imani yangu kuwa wadau wote mlio katika mnyororo huu tutashirikiana kikamilifu katika utekelezaji wa yale yote yaliyomo ndani ya taarifa hii ambayo tunakwenda kuizindua leo hii na katika taarifa zitakazokuwa zinakuja kadri tutakavyosonga mbele." Ameyasema hayo Naibu Katibu Mkuu         

Nae pia Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu alieleza kuwa katika ukaguzi wao walioufanya kwa kipindi hicho walikuta watoto 435 wakitunzwa kwenye Taasisi mbalimbali ambazo zimepewa majukumu kisheria. Na kati yao watoto 46 walikuwa hawajakinzana na sheria ambao wapo mahabusu kwasababu ya wazazi wao wameshikwa kwa makosa mbalimbali ambao pia ni watoto wadogo wasioweza kutenganishwa na wazazi wao. Pia walikuta watoto 260 wapo  kwenye Magereza ambapo kati yao tayari wapo hatiani kutumikia vifungo vyao na wengine kesi zao zilikuwa zikiendelea kwahiyo wapo mahabusu. Na kwa upande wa kwenye shule ya marekebisho watoto waliokuwepo ni 40, kati yao watoto 38 walikuwa ni watoto wa kiume na watoto 2 ni mabinti                                      

Aidha, Mkurugenzi Mwakitalu aliendelea kueleza kuwa katika ukaguzi huo hawakuishia kuona watoto walioko kwenye Taasisi hizo bali walisonga mbele zaidi ili kuweza kufahamu sababu zinazowafanya watoto hawa kuingia kwenye ukinzani na sheria na wakaweza kubaini kuwa chanzo kikubwa ni yalikuwa ni malezi.

"Watoto wengi ambao wameingia katika changamoto hii tumebaini wanatoka katika familia ambazo zina migogoro. Na pia tumebaini kuwa watoto wengi wanaoingia kwenye shida hii ni wale ambao hawapo shule au wanaenda shule kwa kusuasua. Hii yote ni sababu ya kukosa malezi mazuri kutoka kwa wazazi na jamii." Ameyasema hayo DPP.

Pia DPP aliendelea kueleza kuwa wapo watoto ambao kwasababu mbalimbali hawapo pamoja na wazazi wao. Na jamii ina jukumu la kuhakikisha watoto hawa wanapata malezi na kupata haki zao zote za msingi.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi Divisheni ya Utenganishaji wa Shughuli za Mashtaka na Upelelezi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Tumaini Kweka  alieleza kuwa Taarifa hiyo inahusu ukaguzi wa vituo na maeneo ambayo wanashikiliwa watoto waliokinzana na sheria, ambayo inahusu magereza, Mahabusu za  Polisi na inahusu shule maalum za mafunzo ya watoto pamoja na nyumba maalum ambapo watoto hao waliokinzana na sheria wanashikiliwa.                                              

Pia Mkurugenzi Kweka aliendelea kusema kuwa Taarifa hiyo inahusisha zoezi ambalo lilifanyika mwishoni mwa mwaka 2021 pamoja na mwanzoni mwa mwaka 2022 ambapo timu maalum kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ilikwenda kutembelea maeneo hayo chini ya ufadhili wa UNICEF ili kuangalia ni kwa namna gani sheria ya mtoto ya mwaka 2009 inatekelezwa dhidi ya watoto hao ambao wamekinzana na sheria.

Na baada ya ukaguzi huo  timu iliweza kuandaa Taarifa ikiainisha maeneo mbalimbali kuhusiana na utekelezaji wa sheria ya mtoto pamoja na matamko mbalimbali ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa. Na ni kwa namna gani yalikuwa yanatekelezwa katika kuhakikisha haki na ustawi wa mtoto ambae amekinzana na sheria.                                              


Share:

KIKOSI KAZI CHA ULINZI KWA WATOTO DHIDI YA BIASHARA HARAMU YA USAFIRISHAJI WA BINADAMU CHAZINDULIWA

 

Waziri Wa Katiba na  Sheria Mhe. Damas  Ndumbaro  amezindua kikosi kazi cha ulinzi kwa watoto dhidi ya biashara haramu ya Usafirishaji wa binadamu.

Kikosi kazi hicho kimeanzishwa chini ya Mradi wa kupambana na Uhalifu mkubwa wa kupangwa ( Serious Organised Crime- SOC), ambacho kitatekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Akizindua kikosi kazi hicho, Waziri wa Katiba na Sheria, leo Julai 21, 2022 Dkt. Damas Ndumbaro, amesema athari ya uhalifu mkubwa wa kupangwa ni kubwa na inakuwa ya kushtukiza.


"Sisi, Tanzania tunayo mifano hai kuhusu madhara ya uhalifu wa aina hii, kwa mfano uripuaji wa mabomu katika ubalozi wa Marekani uliotekelezwa hapa kwetu, Kenya na Uganda kwa wakati mmoja." Amesema Dkt.  Ndumbaro na kuongeza

Amesema kutokana na mikakati mbalimbali inayotekelezwa na Serikali katika mapambano dhidi ya ukatili na udhalilishaji  wa wanawake na watoto, wameanza kushuhudia kuibuka kwa taarifa kuhusu uhalifu wa aina hiyo katika jamii na umeonesha bayana juu ya kazi kubwa iliyopo katika kukabiliana na janga hilo.

" Kwa maelezo hayo ninajenga hoja kwamba mradi huu wa kupambana na uhalifu mkubwa wa kupangwa hasa ule wa usafirishaji haramu wa Binadamu, unyonyaji na udhalilishaji wa watoto kingono ni muhimu sana na umekuja kwa wakati unaofaa katika nchi yetu" amesema Dkt. Ndumbaro.

Kwa msingi huo, sisi sote tuliopewa dhamana ya kupambana na uhalifu mkubwa wa kupangwa kwa Makosa ya Biashara Haramu ya Binadamu, Ukatili na Udhalilishaji wa Watoto Kingono na Uhalifu Unaovuka Mipaka ya Nchi katika jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hatuna budi kuitumia fursa hii ili kuleta tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yetu ya kuhudumia taifa hili. Huu ni wakati wa kubuni mbinu mbali mbali zitakazoweza kubainisha hila na ghilba za wahalifu pia kubainisha changamoto zinazowakabili wapambanaji wa kazi hii na kutafuta mbinu muwafaka za kukabiliana nazo ili kufikia malengo tuliojiwekea.

Ubunifu wa mbinu mpya ni lazima utekelezwe sambamba na kuongeza uwezo wetu wa teknolojia ya mitandao ambayo baadhi ya wakati inatumika vibaya ili kuwanufaisha wahalifu wanaotaka mafanikio bila ya kufuata na kuheshimu sheria za ndani ya nchi na kimataifa.

" Kwa msingi huu sisi sote tuliopewa dhamana ya kupambana na uhalifu mkubwa wa kupangwa kwa Makosa ya Biashara Haramu ya Binadamu, Ukatili na Udhalilishaji wa Watoto Kingono na Uhalifu Unaovuka Mipaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hatuna budi kuitumia fursa hii ili kuleta tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yetu ya kuhudumia taifa hili." Amesema Dk Ndumbaro na kusisitiza

" Huu ni wakati wa kubuni mbinu mbali mbali zitakazoweza kubainisha hila na ghilba za wahalifu pia kubainisha changamoto zinazowakabili wapambanaji wa kazi hii na kutafuta mbinu muwafaka za kukabiliana nazo ili kufikia malengo tuliojiwekea" amesisitiza.

 

Amesema Ubunifu wa mbinu mpya ni lazima utekelezwe sambamba na kuongeza uwezo wa teknolojia ya mitandao ambayo baadhi ya wakati inatumika vibaya ili kuwanufaisha wahalifu wanaotaka mafanikio bila ya kufuata na kuheshimu sheria za ndani ya nchi na kimataifa.

Akizungumzumzia mradi huu, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania ( DPP) Bw. Slyvester Mwakitalu amesemea mradi huo ni wa miaka minne kuanzia Desemba, 2021 hadi Desemba 2025 na unatekelezwa kwa gharama ya dola za Kimarekani 6,434,320 ambapo zitatumika kwa Tanzania Bara na Zanzibar.

"Mradi huu unatekelezwa kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza na Jumuiya ya Umoja wa Nchi za Ulaya kupitia Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) likishirikiana na UNICEF pamoja na Shirika la Kimataifa la Uhamaji (IOM)" amesema Mwakitalu.

Mwakitalu amesema mradi huo umelenga kujenga uwezo wa kiutendaji kwa taasisi za Serikali zinazohusika katika utekelezaji wa sheria za kupambana na uhalifu mkubwa wa kupangwa ambapo kwa Tanzania Bara utajikita zaidi katika makosa ya biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu na udhalilishaji (unyanyasaji) wa watoto.

"Lengo kuu la mradi huu wa SOC ni kuvijengea uwezo vyombo vya ulinzi na usalama vinavyohusika katika utekelezaji wa sheria za mapambano dhidi ya uhalifu mkubwa wa kupangwa hasa katika nyanja za upelelezi, uendeshaji wa mashtaka na ulinzi kwa wahanga na manusura" Amesema Mwakitalu.

Kwa upande wake, Waziri wa  Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.  Doroth Gwajima amesema uzinduzi wa kikosi hicho umekuja wakati muafaka wakati Serikali ikiendelea kupambana na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.


 

 

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .