• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

UKATILI WA KIJINSIA UATHIRI AFYA NA UCHUMI WA TAIFA - NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA KATIBA NA SHERIA.

Baadhi ya Wakuu wa Mashtaka kutoka Mikoa na Wilaya zote Tanzania bara wakiendelea kufuatilia hotuba ya ufungaji wa Mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya namna ya kukabiliana na kesi za ukatili ambao umekuwa changamoto kubwa kwa sasa nchini.Wa Kwanza Kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini Bw. Joseph Pande, katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara  ya Katiba na Sheria Dkt. Khatib Kazungu akifuatiwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini DPP Bw.Sylvester Mwakitalu wakiwa katika picha ya Pamoja. 

Ukatili wa Kijinsia umetajwa kuwa mojawapo ya chanzo  kikubwa kinachoathiri Afya, Utu, Usalama na Uhuru wa binadam, ambapo  muathirika huwa sehemu ya kunyanyasika kisaikolojia, kimwili, kiafya, na kiakili.Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini DPP Bw.Sylvester Mwakitalu akizungumza na washiriki wa mafunzo ya namna ya kukabiliana na kesi za ukatili wa kijinsia nchini. 

Ukatili huo  hutokana  na vitendo anavyokutana navyo ikiwemo kupata matatizo ya afya ya uzazi, mimba zisizotarajiwa, utoaji wa mimba ambao sio salama, magonjwa ya zinaa, UKIMWI na hata kifo.Naibu Katibu Mkuu,  Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu akizungumza na Waendesha Mashtaka  wa Mikoa, Wilaya, Wapelelezi na Waendesha Mashtaka Viongozi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Naibu Katibu Mkuu,  Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Khatibu Kazungu amebainisha hayo wakati akifungua Mafunzo maalum kwa Wakuu wa Mashtaka wa Mikoa, Wilaya na Waendesha Mashtaka Viongozi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka yanayofanyika mjini Morogoro tarehe 29 Machi, 2023.


Dkt. Kazungu amesema kuwa kuna baadhi ya mila na desturi za kitanzania ambazo zimefumbia macho vitendo vya ukatili wa kijinsia na kubaki kufanya bila kuchukua hatua kali za kisheria hali inayochangia uvunjaji wa haki za msingi za kibinadamu. 


" Tafiti zinaonyesha  ongezeko kubwa la matukio ya ukatili wa kijinsia, ubakaji dhidi ya makundi mbalimbali katika jamii yetu. Hata hivyo bado wahalifu wanaosababisha makosa haya hawajaweza kuwajibishwa ipasavyo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mapungufu katika Upelelezi, mapungufu katika uendeshaji wa Mashauri hayo mahakamani hivyo kupelekea watuhumiwa wengi kuachiwa huru."Amesema Naibu Katibu Mkuu.

Washiriki wa mafunzo wakiendelea kufuatilia mafunzo hayo yaliyofanyika Mkoani Morogoro.

Dkt. Kazungu ameipongezi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa kuona umuhimu wa kutoa mafunzo hayo katika eneo hilo, kwa kuwa kundi hilo ni muhimu katika kufikia malengo ya uendeshaji wa kesi za ukatili hivyo mafunzo hayo yatasaidia katika kushughulikia makosa hayo  kwa Wapelelezi na Waendesha Mashtaka hapa nchini.Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini Bw. Joseph Pande, akizungumza na washiriki wa mafunzo Mkoani Morogoro.

Dkt. Kazungu ameongeza kwa kusema kuwa kazi kubwa inayofanywa na Waendesha Mashtaka nchini ni kuhakikisha waathirika wanapata haki na stahiki zao huku watuhumiwa wakipewa adhabu kali zinazowapa fundisho watu wengine.Katika hatua nyingine Dkt. Kazungu ameitaka jamii kukemea vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa changamoto kubwa sana ikiwemo ubakaji, ulawiti na matendo mengine maovu ambayo ni kinyume cha mila na desturi za Mtanzania.Aidha, Naibu Katibu Mkuu kwa niaba ya Wizara ya Katiba na Sheria alitoa pongezi kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa kuona umuhimu wa kutoa mafunzo hayo katika eneo hilo, sio tu kwa Waendesha Mashtaka lakini pia kwa Wapelelezi kwani mafunzo hayo yatasaidia kuongeza tija katika kushughulikia makosa kwa Wapelelezi na Waendesha Mashtaka katika masuala mazima ya haki jinai.





Share:

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE, UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA MKOA WA SHINYANGA.


Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria (Mb)Florent Kyombo akieleza namna ujenzi wa jengo la Ofisi ya Taifa  ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga litakavyosaidia kutoa huduma kwa karibu kwa wananchi.
         ...................................................................................

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Katiba na Sheria leo tarehe 15 Machi, 2023 imetembelea na kukagua ujenzi wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga ambalo linaendelea kujengwa kwa lengo la kurahisisha zaidi  huduma za kimashtaka kwa wananchi.

Akitoa taarifa za ujenzi wa jengo hilo kwa kamati hiyo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul amesema kuwa mnamo tarehe 26 Septemba, 2022 Ofisi ya Taifa ya Mashtaka iliingia Mkataba na kampuni ya  Mkandarasi Eliroi Construction kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga wenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.15 ikijumuisha ongezeko la thamani VAT.

Mhe. Gekul amesema kuwa mradi huo unatarajiwa  kukamilika ndani ya muda wa miezi 8 ambapo ulianza  kutekelezwa  tarehe 22 Novemba, 2022 mbapo unataraji kukamilika June 22 ambapo mpaka sasa umefikia asilimia 35.Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Pauline Gekul,akitoa taarifa za ujenzi wa jengo hilo kwa kamati hiyo iliyoembelea na kukagua ujenzi wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Aidha Naibu Waziri Mhe. Gekul ameongeza kwa kusema kuwa mpaka sasa Mkandarasi amekwisha lipwa fedha za awali kiasi cha shilingi milioni 323 kati ya bilioni 2.15 huku Mkandarasi Mshauri Mwelekezi wa mradi huo Water Institute kawazulite maombi ya kulipwa kiasi cha shilingi milioni 335.5 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Bw. Sylvester Mwakitalu ameishukuru Kamati hiyo kwa juhudi zake kubwa za kuipigania Ofisi hiyo ambapo kwa mwaka huu wa fedha unaoendelea jumla ya mikoa sita imepatiwa fedha za ujenzi wa Ofisi ikiwa ni pamoja na Shinyanga, Geita, Manyara, Rukwa, Katavi na Njombe na kufanya idadi ya ofisi zinazojengwa kufikia kumi.Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Bw. Sylvester Mwakitalu akieleza namna kamati hiyo imekuwa msaada wa upatikanaji wa fedha za ujenzi wa Ofisi hiyo.

Mkurugenzi Mwakitalu ameushukuru uongozi wa Mkoa wa Shinyanga  chini ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Christine Mndeme kwa kuwapatia eneo la Kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi hiyo ambayo itasaidia na kurahisisha utoaji wa huduma kwa jamii juu ya masuala ya Mashtaka ambapo amesema  eneo hilo awali ilipewa taasisi nyingine.

Mkurugenzi wa Mashtaka aliendelea kueleza kuwa   ujenzi huo utakapokamilika utarahisisha utaoaji wa huduma kwa jamii ambapo watumishi watakuwa na sehemu bora na mazingira rafiki ya utaoji wa huduma.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christine Mndeme ameihadi kamati hiyo kuwa atahakikisha anasimamia kwa ukaribu ujenzi huo ili uweze kukamilika kwa wakati na kuleta tija iliyokusudiwa ya utaoji wa huduma kwa jamii.Kwanza Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Christine Mndeme akiwa pamoja na kamati ya Kudumu ya Bunge, Utawala , Katiba na Sheria.  

Mndeme  ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha hizo kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo kwani ni muhimu kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga huku akiongeza kwa kusema kuwa mradi huo unakwenda kubadili mandhari ya Mkoa wa Shinyanga.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria (Mb)Florent Kyombo  amemtaka mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi kwa kuwa muda aliyopewa mpaka sasa ni zaidi ya miezi minne mradi huo  bado uko asilimia 35 ambapo ulipaswa kuwa asilimia zaidi ya 50.Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria (Mb)Florent Kyombo akisikiliza maelezo ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga.

Kyombo amesema kuwa lengo la ujenzi wa Ofisi hizo ni kusogeza huduma karibu na wananchi hivyo usimamizi Madhubuti unapaswa kuwepo ili kuondoa mikwamo isiyokuwa na tija katika ujenzi huo.Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Bw. Sylvester Mwakitalu akisalimiana na mmoja wa mafundi wanaojenga jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga.

Aidha Kyombo ameipongeza Serikali kwa kutoa fedha  za ujenzi wa Majengo ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka itakayosaidia utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Meneja Mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Ezrael Masawe akitoa maelezo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Utawala, Katiba na Sheria namna ambavyo jeno hilo litakavyojengwa.

Kamati hiyo iko katika ziara ya kukagua na kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

@NPS-HQ

@NPS-Shinyanga 

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .