"Tumieni Mfumo wa NEST ili kuepukana na Changamoto za Manunuzi." Kaimu Naibu DPP

 Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bi. Javelin Rugaihuruza amewataka Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuutumia  Mfumo wa Kielektroniki wa Manunuzi ya Umma (NEST) kwa lengo la kuondokana na changamoto za manunuzi walizokuwa wakikabiliana nazo katika kununua mahitaji mbalimbali ya kiofisi yanayohitajika kufanyika kupitia Mfumo huo.

Kaimu Naibu DPP amebainisha hayo wakati akifungu Mafunzo ya Mfumo wa Kielektroniki wa Manunuzi ya Umma (NEST) yaliyofanyika tarehe 9 Machi, 2024 Mkoani Pwani.

"Niwasihi mtumie siku ya leo kikamilifu ili kuweza kujifunza na kufahamu vema mfumo huu na baada ya kutoka hapa natumaini changamoto zilizokuwepo zitaondoka." Amefafanua hayo Kaimu Naibu Javelin.

Mafunzo ya Mfumo wa Kielektroniki wa Manunuzi ya Umma (NEST) yametolewa kwa Wahasibu na Watumishi wengine wanaofanya kazi za Manunuzi katika Mikoa.



Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .