OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA YACHANGIA UFANISI KATIKA USIKILIZWAJI WA KESI ZA UHUJUMU UCHUMI NCHINI

 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, wakati akiwasilisha hotuba ya Bajeti  ya  Wizara hiyo kwa Mwaka 2025/2026 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,  Leo tarehe 30 April 2025  ameeleza kuwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imechangia ufanisi mkubwa katika uendeshaji wa kesi za Uhujumu Uchumi kwa kipindi kati ya Julai 2024 na Aprili 2025.

Kupitia hotuba yake, Dkt.  Ndumbaro amelieleza Bunge kuwa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  kwa kipindi cha mwaka wa Fedha  2024/2025 iliendesha kesi kubwa 177 katika Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi  ukilinganisha na Kesi 60 pekee zilizoendeshwa katika kipindi  kama hicho kwa mwaka 2023/2024.

Waziri Ndumbaro pia amebainisha kuwa katika Kipindi cha Julai 2024 hadi Aprili 2025, kesi za jinai 27,523 ziliendeshwa katika Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya, tofauti na kesi 25,037 zilizoendeshwa katika Mahakama hizo kwa kipindi  kama hicho kwa  mwaka wa fedha 2023/2024.

Ameeleza zaidi  kuwa, Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeendelea kusogeza huduma kwa wananchi ngazi za Mikoa na Wilaya, ambapo katika kipindi cha mwaka 2024/2025 huduma hizo zimepelekwa kwenye mikoa yote 26 nchini pamoja na  Mikoa minne ya kimashtaka hivyo kufanya idadi ya  mikoa 30 inayopata huduma za Kimashtaka. Sambamba na hilo Waziri Ndumbaro amesema Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imefikisha huduma za mashtaka katika Wilaya 108 nchini.

Ameongeza kusema kuwa, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imekamilisha ujenzi wa majengo yake katika mikoa ya Manyara, Shinyanga, Katavi, Rukwa, Pwani na mkoa wa Kimashtaka Ilala.

Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .