• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

DPP AWATAKA MAWAKILI WA SERIKALI NCHINI KUFUATA MAADILI KWA KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Biswalo Mganga akifungua mafunzo kwa  mawakili 29 wa serikali toka mikoa yote nchini  juu ya kuwajengea uwezo wa Utendaji kazi. 

Mashtaka wa Serikali wameaswa kufanya kazi zao kwa kufuata maadili Ili kuepusha malalamiko kutoka kwa Umma juu ya utendaji kazi wao.

Akizungumza Machi 16, 2021 Jijini Mwanza wakati akifungua mafunzo ya mawakili 39 kutoka katika  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mikoa na Wilaya  ambapo Mkurugenzi wa Mashtaka Bw.Biswalo Mganga amesema kuwa mafunzo hayo yana lengo la kuwajengea uwezo wa utendaji kazi, katika uendeshaji wa kesi za rushwa, utakatishaji fedha na udanganyifu kwa njia ya kimtandao.

Biswalo amesema Dunia ya sasa inaendana na kasi ya mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia hivyo lengo la kuwakutanisha mawakili hawa ni  kuwajengea uwezo,  kubadilishana uzoefu na wakati huo huo kujifunza mbinu mpya za kuenenda na nyakati za mabadiliko.

Bw. Mganga aliendelea kueleza kuwa Taasisi yao inaendelea kufanya kazi ili kuhakikisha kuwa wanapambana kuharakisha kutatua changamoto ya makosa hayo kwa haraka ili jamii iweze kupata haki kwa wakati, na kuwezesha kufanya kazi zao za kimaendeleo kwa wakati.

Biswalo amesema Ofisi ya Taifa ya  Mashtaka pamoja na Waendesha Mashtaka ina changamoto nyingi inazokabiliana nazo hivyo kuwepo kwa mafunzo ya mara kwa mara ni mhimu kwa watendaji hao.

Kwa upande wake Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi Suleiman Nyakulinga amesema kutokana na ongezeko la changamoto ya uhalifu wa kimtandao mafunzo ya mara kwa mara kwa watendaji hao itawasaidia kufahamu namna nzuri ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza.

Nyakulinga ameeleza kuwa  makosa ya Utakatishaji Fedha na Uhalifu wa Kimtandao yameongezeka hivyo kuwa na Waendesha Mashtaka wenye uelewa mkubwa ni mhimu kwa wakati huu.

Naye Wakili wa Serikali toka Mkoani Arusha ambaye amehudhuria mafunzo hayo Bw. Tusaje Samwel amesema kutokana na changamoto zinazojitokeza katika nyanja ya makosa hayo ni mhimu kwao kubadilishana uzoefu na kupata mafunzo ya kuwajengea uwezo ili kuwawezesha kukabiliana na makosa mbalimbali ya kiuhalifu.

Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi Suleiman Nyakulinga akizungumza na washiriki wa mafunzo ambao ni mawakili wa serikali katika ukumbi wa TMDA  Buzuruga Jijini Mwanza 

Baadhi ya mawakili wa serikali toka mikoa yote ya Tanzania Bara wakiendelea kufuatilia kwa ukaribu na umakini  elimu inayotolewa  kuhusiana na uendeshaji wa kesi za rushwa, utakatishaji fedha na udanganyifu kwa njia ya kimtandao
Mkurugenzi wa Mashtaka Biswalo Mganga akiwa na baadhi ya  Wakurugenzi wa Idara katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka jijini Mwanza wakati wa mafunzo ya kuhusiana na uendeshaji wa kesi za rushwa, utakatishaji fedha na udanganyifu kwa njia ya kimtandao
Baadhi ya mawakili wa serikali toka mikoa yote ya Tanzania Bara wakiendelea kufuatilia kwa ukaribu na umakini  elimu inayotolewa 

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Usimamizi wa Kesi na Uratibu wa Upelelezi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambaye anashughulikia Usimamizi wa Kesi Bw. Tumaini Kweka akizungumza  na washiriki wa mafunzo hayo jijini Mwanza 

Share:

WANANCHI WATAADHALISHWA KUJIHUSISHA NA BIASHARA HARAMU YA UPATU

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini akiwa na Wakuregenzi wa idara mbalimbali toka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka akiendelea kuzungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.

Na Mwandishi NPS 

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw Biswalo Mganga amewataka Wananchi kujiepusha na kujihusisha na biashara haramu ya upatu kwakuwa ni kosa la Jinai kwa mhamasishaji na mtoaji fedha.

Bw. Mganga ameyasema hayo leo katika kikao chake na vyombo vya habari kilichofanyika jijini Dodoma ambacho alikitumia kuelekeza na kuelimisha umma kutokana na kuibuka upya kwa biashara ya upatu unaojitokeza katika siku za hivi karibuni.

Alisema vitendo vya ushiriki katika biashara haramu ya upatu ( pyramid schemes) vinakiuka masharti ya Sheria ya Benki na Taasisi za Kifedha Na.5 ya Mwaka 2006 inayokataza mtu yeyote kupokea.miamala ya Kifedha kutoka kwa umma bila leseni na ni kosa la Jinai siyo tu kwa anayehamasisha na kupokea fedha bali hata kwa wanaotoa fedha hizo.

Alisema wanaofanya na kushiriki katika biashara hiyo wapo katika hatari ya kupoteza fedha zao pamoja na kushtakiwa Mahakamani kwa kosa la kushiriki biashara haramu ya upatu.

Alisema Umma unakumbushwa kuwa mipango.kama hii ya kilaghai imewahi kujitokeza siku za nyuma na kusababisha wananchi wengi kupoteza fedha zao ambapo aliitaja baadhi ya mipango hiyo danganyifu kuwa ni.pamoja na Rifaro Africa, IMS, D9, miradi ya kuku kupitia kampuni ya Mr. Kuku na Development Enterpreneurship Initiative ( DECI).

Alisema mipango hiyo kwasasa imeibuka na sura Mpya kama Biashara y Kimtandao ambapo wananchi wanaalikwa kushiriki kwa kuwashawishi wengine kujiunga

Mkurugenzi wa Mashtaka amesema kwa kuzingatia masharti yaliyoainishwa katika Ibara ya 59B ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 na vifungu vya 8 na 9(1)(c) vya Sheria ya Usimamizi wa Mashtaka (Sura 430 Marejeo 2019) 

ambapo ametoa maelekezo ya vyombo vyote vya Upelelezi kutorejesha fedha kwa watu walioshiriki katika makosa ya upatu ambapo ameeleza kuwa utaratibu wa kurejesha mali za wahanga au kutaifisha mali zinazohusiana na Uhalifu umeainishwa katika Sheria mbalimbali na hivyo kuwataka wale wote wanaotaka kurejesha fedha au mali zinazohusiana na Uhalifu kwa wahanga kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Sheria

 

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .