• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

MAGEREZA YAPONGEZA TAASISI ZA HAKI JINAI KWA UTENDAJI MZURI

 Mkuu wa gereza Kuu Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza Juma Mwaibako ametoa pongezi kwa taasisi zinazounda mnyororo wa haki jinai kwa utendaji mzuri ambao umeleta tija kubwa na kupunguza sana msongamano wa Mahabusu gerezani.

 Aidha amepongeza pia ushirikiano wanautoa katika uendeshaji wa mashauri ya jinai kupitia kaguzi za UTATU zinazofanyika katika gereza hilo ambazo zimesaidia haki kupatikana kwa kesi nyingi kukamilishwa upelelezi na kusikilizwa mahakamani.

Kamishna Msaidizi wa Magereza amebainisha hayo wakati wa ziara ya Mkurugenzi wa Mashtaka akiwa  ameambatana na  Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Cyprian Chalamila na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya Bw. Aretas Lyimo walipotembelea Gereza Kuu Ukonga tarehe 20 Novemba, 2024 ikiwa ni muendelezo wa ziara ya siku tatu ya kutembelea magereza katika Mkoa wa Dar es saalam.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Cyprian Chalamila amesema kuwa changamoto zote zilizowasilishwa zimepokelewa na zitafanyiwa kazi mapema iwezekanavyo.  

Akiongea na wafungwa wa gereza hilo amesema “Tunashukuru kusikia kwamba mmejifunza mengi mazuri mkiwa hapa na mkitoka mtaenda kuwa raia wema na tunawaahidi kuwa changamoto mlizoziwasilisha kwetu zitafanyiwa kazi na mtapata mrejesho ndani ya wiki mbili tangu leo.” 

Aidha, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya Bw. Aretas Lyimo, ameeleza kuwa, kupitia changamoto zilizopokelewa katika ziara hiyo imesaidia kupima utendaji kazi wao  na utendaji wa wale waonaowasimamia ambapo amesema “Ziara hii imekuwa chachu kubwa kwetu ya kuboresha sehemu zenye changamoto ili kuhakikisha haki za mahabusu na wafungwa zinalindwa ipasavyo”.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu wakati akihitimisha ziara ya kutembelea magereza ya mkoa wa Dar es saalam, ameipongeza timu nzima ya haki jinai Jijini Dar es salaam kwa kupunguza msongamano wa Mahabusu katika gereza la Ukonga ikilinganishwa na mwaka uliopita. 

Akizungumza na timu aliyoambatana nayo katika ziara hiyo DPP Mwakitalu amesema “Tukikamilisha upelelezi na uendeshaji wa kesi kwa wakati itasaidia kuwapunguzia mzigo wanaowatunza mahabusu na kuondoa msongamano gerezani, hivyo niwatie moyo wa kuendelea kuwahudumia wananchi kwa misingi ya haki.”



Share:

DPP AAHIDI KUSHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZA MAHABUSU GEREZA LA KEKO

 Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu ameahidi kushughulikia changamoto na kero zinazowakabili mahabusu na wafungwa waliopo katika gereza la keko Jijini Dar es saalam.

DPP Mwakitalu amebainisha hayo tarehe 19 Novemba, 2024 mara  baada ya kukagua na kuzungumza na mahabusu waliopo katika gereza hilo.

Katika hatua nyingine Bw. Sylvester Mwakitalu, amesema kuwa mazungumzo yaliyofanyika na mahabusu katika gereza hilo yamekuwa yenye manufaa makubwa kwani yatasaidia kurekebisha na kuboresha utendaji wa kazi na changamoto zote zilizowasilishwa zitashughulikiwa mapema na kwa masuala yanayohitaji mabadiliko ya sheria nayo yatawasilishwa katika Mamlaka husika ili yaweze kushughulikiwa.

Akizungumza na vyombo vya habari Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Aretas Lyimo, ametoa onyo kwa watuhumiwa watakaoachiwa au kumaliza vifungo vyao kutorudia kutenda makosa bali wasaidiane na serikali katika kuiletea nchi maendeleo na wafanye kazi halali ili kujiongezea kipato.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Cyprian Chalamila amesema kuwa lengo kuu la ziara hiyo ni kupokea changamoto zinazowakabili watuhumiwa waliopo katika mahabusu hiyo na kuchukua hatua za kushughulikia changamoto zilizowasilishwa ili sio tu haki itendeke bali ionekane ikitendeka.

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Bw. Ramadhani Kingai amesema kuwa atashughulikia changamoto za kiupelelezi ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati.

Naye Mkuu wa gereza la Mahabusu la Keko, Kamishna Msaidizi Juma Mgumba amemshukuru Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu na timu aliyoambatana nayo katika ziara huku akieleza kuwa upelelezi ukikamilishwa mapema na kesi zikasikilizwa na kuisha kwa wakati itasadia watuhumiwa kujua hatma yao  na msongamano katika gereza hilo kupungua au kuisha kabisa.



Share:

MAHABUSU WAMPONGEZA DPP KWA KUPUNGUZA MSONGAMANO SEGEREA

 Mahabusu na wafungwa kutoka Gereza la Mahabusu Segerea wamempongeza Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu kwa kupunguza msongamano wa Mahabusu na wafungwa waliopo katika gereza hilo tofauti na hali ilivyokuwa awali.

“Mwaka 2021 ulipotutembelea katika gereza hili tulikuwa mahabusu na wafungwa zaidi ya elfu mbili lakini leo mahabusu na wafungwa idadi yetu ni mia tisa na kidogo, kwa kweli tunakushukuru sana kwa kushughulikia kesi zetu na kufanya mrundikano kupungua humu gerezani”. 

Mahabusu na Wafungwa wamebainisha hayo wakati Mkurugenzi wa Mashtaka alipofanya ziara ya kutembelea gereza hilo kwa lengo la kuongea na kusikiliza kero za mahabusu na wafungwa hao.

Kwa upande wake Bw. Mwakitalu ameeleza kuwa licha ya kazi nzuri inayofanywa katika mkoa wa Dar es saalam, bado inatakiwa kuongeza kasi ya ukamilishaji wa upelelezi na uendeshaji wa mashtaka na kuhakikisha kesi zinazopelekwa mahakamani zinakuwa zenye ushahidi utakaoleta ushindi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Crispin Chalamila alisisitiza juu ya kuongeza kasi katika kushughulikia kesi kwa wakati ili kuepusha malalamiko huku akihimiza kuwa haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa.

Aidha, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti  na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Aretas Lyimo alisema kuwa kesi zinazohusiana na madawa ya kulevya ambazo upelelezi haujakamilika aliahidi kuzishughulikia na kukamilisha upelelezi wake kwa wakati.



Picha ya pamoja ikijumuisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Crispin Chalamila, Kamishna Generali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Aretas Lymo wakiwa na viongozi wa ngazi ya mkoa wanaounda mnyororo wa Haki Jinai, Waendesha Mashataka kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kutembelea gereza la Mahabusu Segerea Jijini Dar es salaam

Share:

DPP ATEMBELEA MAGEREZA JIJINI DAR ES SALAAM.

 Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu, afanya ziara ya siku tatu ya kutembelea magereza ya mahabusu Mkoa wa Dar es saalam kwa lengo la kuongea na kusikiliza changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo mahabusu na wafungwa ili kuweza kuzifanyia kazi kwa wakati.

Katika ziara hiyo,  Bw. Mwakitalu aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Crispin Chalamila, Kamishna Generali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Aretas Lyimo, viongozi ngazi ya mkoa wanaounda mnyororo wa Haki Jinai pamoja na  Waendesha Mashataka kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Ziara hiyo inafanyika tarehe 18-20 Novemba, 2024 Jijini Dar es salaam.



Picha ya pamoja ikijumuisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Bw. Crispin Chalamila, Kamishna Generali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Bw. Aretas Lymo wakiwa na viongozi wa ngazi ya mkoa wanaounda mnyororo wa Haki Jinai, Waendesha Mashataka kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kutembelea gereza la Mahabusu Segerea Jijini Dar es salaam

Share:

DPP ASISITIZA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA.

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Bw. Sylvester Mwakitalu ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza  la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza hilo unaofanyika katika Ukumbi wa Kwatunza Beach uliyopo Ilemela Jijini Mwanza kuanzia Octoba  31 hadi Novemba 1.   


Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Bw. Sylvester Mwakitalu amewaasa watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa kuzingatia maadili na kanuni za utumishi wa Umma ili kuwezesha upatikanaji wa haki kwa wakati.

Bw.Mwakitalu amebainisha hayo wakati akifungua Mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika katika ukumbi wa Kwatunza Beach uliopo Ilemela  Jijini Mwanza leo Oktoba 31, 2024 ambapo amesema kuwa licha ya wafanyakazi kudai maslahi na stahiki zao ni vema wakatimiza wajibu wao kwa wakati na kwa ufanisi.

Nasisitiza uwajibikaji katika kazi zenu na katika kikao hiki msiwaangushe wenzenu waliobaki kwenye vituo vyenu vya kazi, kwa kuhakikisha mnatoa mapendekezo, maoni  na kueleza changamoto zao ili kuwezesha kikao hiki kutoka na maazimio ya pamoja yatakoyowezesha kuweka mazingira bora ya utendaji kazi wetu na masuala yote yanaohusu utumishi” amesema Bw. Mwakitalu Mkurugenzi wa Mashtaka.

Aidha, Mwakitalu amesema uwepo wa Baraza la Wafanyakazi katika taasisi ni moja ya njia bora ya kupokea, kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wafanyakazi katika maeneo mbalimbali ya kazi kutokana na jiografia ya nchi na hivyo kupitia wawakilishi wao kwenye baraza inalenga kuleta mitazamo chanya na kuboresha maisha ya watumishi.

Katika hatua nyingine Bw. Mwakitalu ameitumia nafasi hiyo kumkaribisha Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo Bi. Bibiana Kileo ambaye ameteuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini ambaye kimuundo wa baraza anaingia moja kwa moja kuwa Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

Naye Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo amesema tangu kuasisiwa kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mwaka 2018 Ofisi imekuwa ikijadili na kupitia masuala mbalimbali yanayaohusu wafanyakazi ili kutathmini na kuona ni kwa namna gani Ofisi imeweza kutekeleza maazimio ya mabaraza yaliyopita

Bibiana amesema Baraza la Wafanyakazi husaidia kuwapa nafasi ya kutafakari masuala mbalimbali yanayowahusu zikiwepo  changamoto zao  ili kuwawezesha kufanya kazi zao kwa kuzingatia weledi na umahiri walionao sambamba na kuwapongeza watumishi wote kwa kufanya kazi kwa moyo wa uaminifu ili kusaidia jamii kupata haki zake.

Akizungumza katika Mkutano huo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Simon Ntobi amesema baraza hilo la tatu la wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka lina jukumu kubwa la kuishauri taasisi ili maslahi ya wafanyakazi yaweze kupatikana kwa wakati.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa Bw. Rugemalira Rutatina ameipongeza Ofisi ya Mashtaka kwa kulipa hadhi Baraza la Wafanyakazi kwa kuhakikisha wanapokea na kupitia changamoto za wafanyakazi  katika mazingira rafiki na kuwapa nafasi ya kueleza  changamoto zao ili tija na ufanisi wa kazi uweze kuonekana.

Rugemalira amewasisitiza wakuu wa Divisheni kuwahamasisiha wafanyakazi walio chini ya idara zao kujiunga na mabaraza ya wafanyakazi ili waweze kutoa maamuzi ya pamoja na si kungoja kuamriwa na kundi la wachache ambao ni wanachama hai wa baraza.

Kwa upande wake Afisa Kazi Mkuu Kanda ya Kati, Bw. Goodluck Luginga akizungumza kwa niaba ya Kamishna wa Kazi katika Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka amesema ni jukumu la watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  kufanya kazi kwa tija ili kuleta matokeo chanya kwa ajili ya umma.

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Bw. Sylvester Mwakitalu ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza  la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza hilo unaofanyika katika Ukumbi wa Kwatunza Beach uliyopo Ilemela Jijini Mwanza kuanzia Octoba  31 hadi Novemba 1.Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bi. Bibiana Kileo akitoa salamu fupi na kumkaribisha Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la ofisi hiyo Bw. Sylvester Mwakitalu kufungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika tarehe 31 Oktoba hadi 01 Novemba, 2024 Jijini Mwanza.Mkurugenzi wa  Utawala na Raslimaliwatu wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Simon Ntobbi akimkaribisha Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo kutoa salamu kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika tarehe 31 Oktoba hadi 01 Novemba, 2024 Jijini Mwanza.
Naibu Katibu Mkuu Tughe Taifa Bw. Rugemalira Rutatina akitoa salamu na nasaha kutoka TUGHE wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika tarehe 31 Oktoba hadi 01 Novemba, 2024 Jijini Mwanza.
Afisa Kazi Mkuu wa Kanda ya Dodoma Bw. Goodluck Luginga  akiwasilisha mada juu ya  Haki na Wajibu wa Wafanyakazi wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika tarehe 31 Oktoba hadi 01 Novemba, 2024 Jijini Mwanza.
Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Juma Kattanga akitoa neno la ukaribisho na utambulisho katika  Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika tarehe 31 Oktoba hadi 01 Novemba, 2024 Jijini Mwanza.
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Makosa dhidi ya Binadamu na Utangamano wa Taifa  kutoka Ofisi ya Mashtaka akiongoza Shughuli ya  Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi  wa Ofisi hiyo unaofanyika Mkoani Mwanza.
Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. Samwel Nyungwa akiwasilisha mada juu ya Nafasi na Umuhimu wa Baraza la Wafanyakazi mahali pa kazi wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika tarehe 31 Oktoba hadi 01 Novemba, 2024 Jijini Mwanza.


Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa Mashtaka wakiendelea kufautilia Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa  ya Mashtaka unaofanyika Jijini Mwanza.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa Mashtaka wakiendelea kufautilia Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa  ya Mashtaka unaofanyika Jijini Mwanza.

Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa Mashtaka wakiendelea kufautilia Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa  ya Mashtaka unaofanyika Jijini Mwanza.

Picha ya pamoja ikijumuisha Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  Bw. Sylvester Mwakitalu (katikati) Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bi. Bibiana Kileo (wa pili kushoto) pamoja na wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka unaofanyika tarehe 31 Oktoba hadi 01 Novemba, 2024 Jijini Mwanza





Share:

WATUMISHI WAASWA KUYAENZI MAZURI YA MAREHEMU MAUGGO

 Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mhe. Juma Chikoka amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi kwenye mazishi ya Marehemu Peter Mauggo aliyekuwa Mtumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma yaliyofanyika tarehe 24 Oktoba, 2024 katika kijiji cha Kurugee, Majita wilaya ya Musoma Mkoani Mara.

Akitoa salamu za pole za Mhe. Kanali Mtambi, Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa pole kwa wafiwa wote, ndugu, jamaa na marafiki na kuwasihi kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu  cha msiba huo na waendelee kumwombea Marehemu Peter Mauggo ili Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi.

"Hili jambo lililotokea sisi wengine tunatoa tu pole lakini mfariji mkubwa ni Mwenyezi Mungu, kwahiyo kila jambo tumtumainie na tumtegemee yeye. Kila jambo tunalolifanya tumtangulize Mungu mbele.”Amebainisha hayo Mhe. Juma.

Katika hatua nyingine Mhe. Chikoka amesema umati mkubwa umejumuika mahali hapo kutoa pole kwa wafiwa kwa sababu Marehemu alikuwa ni mtu ambae aliishi na watu kwa amani na upendo hivyo kupitia kifo chake ameacha alama ndani ya mioyo ya watu.




Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .