MKURUGENZI WA MASHTAKA AZINDUA TOVUTI YA CHAMA CHA WAENDESHA MASHTAKA AFRIKA MASHARIKI

 Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Biswalo  Mganga amezinduzi Tovuti ya  Chama cha Waendesha  Mashtaka Afrika Mashariki akishirikiana na viongozi wengine kutoka katika  nchi wanachama.

uzinduzi huo umefanyika Novemba 16, 2020 kwa njia ya Mtandao ambapo Mkurugenzi wa Mashtaka nchini biswalo mganga  ameedesha zoezi hilo akiwa jijini Dodoma huku   Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Kenya  ambaye pia ni Katibu wa chama hicho Bw. Noordin Mohamed Haji  akiwa jijini Nairobi.

 katika uzinduzi huo viongozi mbalimbali wameshiriki akiwemo  Bi. Heather Schildge ambaye  ni    Naibu  Mkurugenzi wa  Misioni kutoka Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani-USAID, Bi. Julie Thomson ambaye ni Mkurugenzi wa Trafiki  Progamu ya Afrika, Wawakilishi Kutoka katika Mashirika ya Kimataifa na Kikanda pamoja na Waendesha Mashtaka kutoka  baadhi ya nchi wanachama wa Umoja huo.

Akieleza umuhimu wa  Tovuti hiyo Bw. Biswalo alisema uzinduzi huo ni miongoni mwa hatua muhimu iliyofikiwa katika  kuimairisha mapambano dhidi ya uhalifu wa wanyamapori  katika nchi za Afrika Mashariki.

Chama Cha Waendesha Mashtaka wa Afrika Mashariki kilianzishwa mwaka 2010 kikiwa na jumla ya wananchama kutoka nchi tano ambazo ni Tanzania, Rwanda, Burundi, Sudani ya Kusini na Kenya ambapo hadi  kufika hivi sasa chama hicho kimefanikiwa kuongeza wanachama kutoka nchi nyingine jirani zikiwemo Somalia, Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Sudan, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, Zambia, Malawi na Msumbuji.

Wakati wa Uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Mashtaka aliendelea kueleza kuwa katika kipindi cha mwaka 2009 hadi 2014 katika nchi ya Tanzania idadi nyingi ya Tembo ilishuka hadi kufikia asilimia 60 kutokana na ujangili na biashara haramu ya wanyamapori ukilinganisha na matukio ya nchi nyingine za jirani.

''Tovuti hii ni chombo muhimu kwa ajili ya kuhakikisha masuala yote ya taarifa dhidi ya uhalifu wa Wanyama katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa yanarahisishwa ili kupambana na wale wote wanaojihusisha na biashara haramu za Wanyamapori   pamoja na kuimarisha mifumo wa mawasiliano katika nchi wanachama''.

''Ni matumaini yangu kuwa website hii kupitia umoja wa waendesha mashtaka wa masuala ya wanyama na mazingira utaamsha katika matumizi ya sheria mbalimbali za kikanda za wanyama kupelekea kukua kwa uhifadhi wa wanyama na kuwa na kituo cha kutolea taarifa kuhusu makosa hayo''.

''Napenda kushukuru waendesha mashtaka wote kwa ushiriano waliotoa katika kutengeneza na kuanzisha tovuti na juhudi za makusudi za kujenga umoja huu''.amesema Bw Biswalo Mganga

Mwisho aliwashukuru wajumbe waliohudhuria katika kikao hicho wakiwemo Bw. Noordin Mohamed Hji, Bi. Heather Schildge, Bi. Julie Thomson, na wawakilishi mbalimbali kutoka Mataifa mbalimbali ya Kiserikali.

 

Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .