AYUBU KIBOKO NA MKEWE PILLY KIBOKO WAHUKUMIWA JELA MIAKA 20 KWA KUKUTWA NA DAWA ZA KULEVYA

 

Pichani ni Ayubu Mfaume  Kiboko akiwa pamoja na Mke wake Pilly Mohamed Kiboko baada ya kuhukumiwa  kutumikia kifungo cha Miaka 20 Jela. 
NA MARRYGORETH NTANDU ...

Mahakama Kuu Kitengo cha Uhujumu Uchumi Kanda ya Dar es salaam  imemtia hatiani mshtakiwa Ayubu Mfaume Kiboko pamoja na mke wake Pilly Mohamed Kiboko na kuhukumiwa kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya.

Kesi hiyo Na.13/2019,   imetolewa  hukumu  Desemba 18, 2020   mbele ya Mhe. Jaji Lilian Mashaka ambapo Imeelezwa  Mahakamani hapo kuwa mnamo tarehe 23 Mei, 2018 mshtakiwa huyo pamoja na mke wake walikamatwa na Maafisa wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya mara baada ya kufanya upekuzi wa nyumba yao iliyopo eneo la Tegeta Nyuki Jijini Dar es salaam.

Katika  upekuzi huo walifanikiwa kupata Madawa  ya kulevya aina ya Heroid Hydrochloride yenye ujazo wa Gram 251.25
Baada ya kupatikana kwa madawa hayo washtakiwa hao walishtakiwa kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya chini ya kifungu cha 15(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya.

Katika kuthibitisha shtaka hilo upande wa Jamhuri uliwaita mashahidi 6 na kutoa vielelezo 16 ambapo upande wa utetezi washtakiwa walijitetea wenyewe na kutoa vielelezo viwili.
Baada ya kupitia ushahidi huo kwa ujumla wake, mahakama imejiridhisha kwamba Jamhuri imethibitisha shtaka bila kuacha shaka, hivyo  kuwatia hatiani washtakiwa  wote wawili.

Kesi hiyo imeendeshwa na Mawakili wa Serikali Faraja Nchimbi, Salim Msemo, Costantine Kakula, Candid Nasua pamoja na Tully Helela.

Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .