SITA WAHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 3 AU KULIPA FAINI YA LAKI TANO KILA MMOJA BUKOBA ,18 WAFUTIWA MASHTAKA PWANI

BUKOBA-KAGERA 

 Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba katika Shauri Na. Ec 05/2020 imewatia hatiani washtakiwa sita akiwepo Deziderius Dominician na wenzake watano kwa kosa la  kupatikana na nyavu haramu za uvuvi wa Samaki na kuwapa adhabu ya kulipa faini ya Shilingi Laki tano (500,000/=) kila mmoja au kwenda jela miaka mitatu pamoja na kutaifishwa mali zao zilizotokana na makosa ya uhalifu waliyoyafanya.

Hukumu hiyo imetolewa tarehe Desemba 30  baada ya washtakiwa kukiri Makosa na kuingia makubaliano  na  Mkurugenzi wa Mashtaka  ambayo ni (plea bargaining) .

Katika shauri hil0  Mahakama pia imewaamuru washtakiwa kuilipa  Serikali fidiia ya  kiasi cha shilingi Milioni Hamsini ambapo washtakiwa wamelipa  fedha hizo  kupitia  akaunti ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) iliyopo Benki Kuu ya Tanzania (BOT).

Sambamba na amri hizo  Mahakama pia imetoa amri ya kutaifishwa mali za washtakiwa zikiwepo gari aina ya Mitsubishi Canter lenye namba ya usajili T.683 CPL , Nyumba ya kulala Wageni, Nyumba ya kupangisha, Kiwanja kilicho na Mashine ya Kusaga na Kukoboa vyote vikiwa na thamani ya Shilingi za kitanzania Milioni Mia Moja na Hamsini na Tisa (159,000,000/=)

Kesi hiyo imeendeshwa na Wakili wa Serikali  Shomari Haruna


Mwonekano wa Mbele wa  Gereza la Mahabusu lililopo Mkuza Wilayani Kabaha Mkoani Pwani.

KIBAHA-PWANI 

Wakati huo huo Jumla ya Washtakiwa Kumi na Nane (18) wamefutiwa Mashtaka  na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Biswalo Mganga na kuachiliwa huru na Mahakama baada ya kutembelea Gereza la Mkuza lililopo wilayani Kibaha Mkoani Pwani hivi karibuni.

Zoezi hilo limefanyika Desemba  30, 2020 baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka kutembelea gereza hilo na kujionea hali halisi.

Baada ya kuwafutia Mashtaka, Mkurugenzi wa Mashtaka aliwataka washtakiwa hao walioachiwa huru wanaporudi uraiani, kuhakikisha   wanaenda kuwa raia wema.

Tembelea Mitandao yetu ya kijamii ikiwemo instagram,youtube,tovuti 

Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .