WASHTAKIWA 183 WAFUTIWA MASHTAKA MKOANI KAGERA DPP AWAONYA KUTORUDIA MAKOSA TENA

Katikati  ni Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini Bw. Biswalo Mganga  akikata utepe wa ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya  Karagwe akiwa na Mkuu wa wilaya hiyo Mheshimiwa Godfrey Mheluka pamoja na Viongozi wengine waliohudhuria Sherehe hizo za Ufunguzi wa ofisi. 
                   Na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.
Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) Biswalo Mganga amewafutia Mashtaka jumla ya washtakiwa 183 katika magereza ya Karagwe, Bukoba, Biharamulo na Muleba mkoani Kagera.

Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP).Biswalo Mganga amebainisha hayo wakati akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Karagwe mkoani Kagera ambapo amesema kuwa mkoa huo unakabiliwa na kesi nyingi za mauaji.

Biswalo ameeleza  baada ya kutembelea magereza mbalimbali  na kuongea na mahabusu walioko ndani ameamua kuwafutia washtakiwa  57 toka wilaya ya  Karagwe, 54 Bukoba, 48 Biharamulo  na Muleba 26 huku katika ziara hiyo akikutana na badhi ya washtakiwa ambao ni wahamiaji haramu 15  waliokuwa wamekaribishwa na wazawa wa mkoa wa Kagera.

"Kimsingi kuna makosa mengi na kesi nyingi ambazo walengwa hawastahili kuwemo gerezani hivyo nimeamua kuwaachia kikubwa niwaombe viongozi wa dini muendelee kuhubiri amani,upendo ili vitamalaki kwani vitasaidia kupunguza hizi kesi"amesema Mganga.

Aidha, Bw.Biswalo  ametanabaisha kuwa hatosita kumchukulia hatua mtu yoyote bila kujali nafasi aliyonayo kisiasa,dini au Serikali ikigundulika kuwa amejihusisha   na vitendo vya Uhalifu ambapo amesisistiza suala la amani ni jukumu la kila mtu hivyo wanawajibika kuitunza kwa kuepuka kufanya makosa ya jinai.

Hata hivyo, Bw. Biswalo amewataka wahusika wote wenye jukumu la kuendesha Mashtaka kutoka Taassi ya kuzuia na kupambana na Rushwa(TAKUKURU), Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania(TANAPA) na Polisi wote kutumia Ofisi ya Taifa ya  Mashtaka ya wilaya hiyo kinyume cha hapo hatasita kuwanyanganya nyenzo alizowapatia za kibali cha  kuendesha Mashtaka kwa Niaba ya Mkurugenzi wa Mashtaka.

"Ninawaagiza waendesha Mashtaka wote wa wilaya hii kuanzia leo majarada yote nataka  leo yahamie kwenye ofisi hii ,na wote mnaohusika na kuendesha mashtaka uwe Tanapa,Takukuru mtakuwa chini ya Mwanasheria huyu Haruna Shomari na atakayekwambia mimi nipo chini ya DCI niambie sitasita  kumtengua na nitamnyanganya nyenzo zangu."amesma DPP Mganga.

Kwa upande wake Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Kagera Mhesimiwa Ntemi Kilekamajenga amesema mkoa wa  Kagera unaongoza kwa kuwa na kesi nyingi za mauaji ambapo amewaomba viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani ili kupunguza vitendo vya uhalifu.

Jaji Ntemi amesema  kesi nyingi zinaweza kuishi kwa  njia ya usuluhishi nje ya mahakama hivyo kuipunguzia Serikali gharama za uendeshaji  wa kesi. 

Aidha, Jaji Ntemi amesema mkoa wa Kagera  kesi ambazo zipo katika hatua ya kusikilizwa zinakaribia kuvuka 450 hivyo mkoa wa Kagera  unaweza kuwa wa pili au watatu kwa Tanzania kuwa na kesi nyingi za mauaji

Askofu wa Jimbo  Katoliki la Kayanga Mhasham, Almachius Rweyongeza  amebainisha kuwa  kufunguliwa kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  katika wilaya ya Karagwe kutasaidia wananchi kupata haki kwa wakati sambamba na kuwakumbusha viongozi wenzake wa dini kutimiza wajibu wao wa kuhubiri upendo na amani kwa mujibu wa maandiko matakatifu.

Mwakilishi wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) mkoa wa Kagera Liberatha  Bamporiki ameeleza kufunguliwa kwa Ofisi hiyo ya Mashtaka katika wilaya ya Karagwe  kutapunguza gharama na muda mwingi waliokuwa wakiutumia kwenda Manispaa ya Bukoba kufautilia kesi zao hali itakyoaaidia kasi ya mashauri kuongezeka na kusaidia kukamilika kwa wakati

Nao baadhi ya wakazi wa Karagwe akiwemo Clemence Isherenguzi na Selestine John wamesema kuwa kufunguliwa kwa ofisi hiyo ni ukombozi kwao kutokana na awali walikuwa wakitumia gharama kubwa kusafiri toka Karagwe kwenda Manispaa ya  Bukoba umbali mrefu kufuata huduma za Mashtaka ambapo kwa sasa uwepo wa ofisi hiyo utasaidia kupunguza mzigo wa gharama  kwa wananchi wa wilaya ya Karagwe.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw.Biswalo Mganga akihutubia katika hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Karagwe, mkoani Kagera
Baadhi ya Viongozi wa Dini pamoja na Wananchi  Wilayani Karagwe Mkoani Kagera wakiwa wameketi wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ofisi ya Mashtaka wilayani humo Januri 21.
Baadhi ya Watumishi  kutoka idara mbalimbali za Serikali wakiwa wameketi wakifuatilia hotuba za viongozi wakati wa hafla ya  ufunguzi wa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Karagwe.  
Wakazi wa mji wa Kayanga-Karagwe waliofika kushuhudia ufunguzi wa Ofisi ya  Taifa ya Mashtaka wilayani humo wakiendelea kufuatilia masuala mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa na viongozi wa Serikali na Dini.
Askofu wa Jimbo  Katoliki la Kayanga Mhasham, Almachius Rweyongeza akizungumzia namna ambavyo viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kukuza na kuimarisha amani kwa kuhubiri ujumbe wa upendo,umoja na mshikamano nyakati zote hali itakayochangia kupungua kwa vitendo vya uhalifu.
Mkuu wa wilaya ya Karagwe mkoani Kagera Godfrey Mheluka akisisitiza jambo kwa wakazi wa wilaya hiyo kuitumia vema Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambayo uwepo wake Utasaidia kupunguza malalamiko na kero zao. 
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw.Biswalo Mganga akisalimiana na Askofu wa Jimbo Katoliki la Kayanga Mhashamu Almachius Rweyongeza kabla ya ufunguzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilayani Karagwe Januari 21.
Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakifuatilia maelezo na hotuba za viongozi.  
Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Rebecka Kwandu akiendelea kufutilia hotuba za viongozi mbalimbali. 
Wageni waalikwa wakiendelea kufuatilia  hotuba za Viongozi  mbalimbali. 
Wageni waalikwa wakiendelea kufuatilia  hotuba za Viongozi  mbalimbali. 

Mwonekano wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Karagwe  mkoani Kagera kabla ya ufunguzi wake. 
Wakazi wa Kayanga-Karagwe wakiwa wamesimama wakishuhudia ufunguzi wa ya Mashtaka wilaya ya Karagwe. 
 
Wa nne toka kushoto, ni Mkurugenzi wa Mashtaka  Bw.Biswalo Mganga akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Edson Makallo, Mkuu wa wilaya ya Karagwe Mheshimiwa Godfrey Mheluka, Askofu wa Jimbo Katoliki  Kayanga Mhasham Almachius Rweyongeza, watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na wajumbe wa kamati  ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo.




Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .