OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA YASAINI MAKUBALIANO (MOU) DHIDI YA KUKABILIANA NA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU

 Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu kulia akibadilishana Hati ya Makubalino (MOU) na  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) kushoto baada ya kusaini Makubaliano hayo  juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu . Makubaliano hayo yamefanyika leo Januari 24,2024 Jijini Mwanza.

MWANZA-

Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeingia Makubaliano (MOU) na Shirika  lisilo la Kiserikali la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) juu ya utekelezaji wa Mradi wa Kukabiliana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu katika maeneo ya Upelelezi na Mashtaka.

Makubalianao hayo yamefanyika leo Jijini Mwanza kati ya Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanasheria           Wasio na Mipaka (Lawayers Without Borders) Bi  .Roben Tylor.

Akizungumza kabla ya kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu amesema kuwa moja ya ajenda za kukabiliana nazo ni uhalifu wa kusarifisha binadamu kinyume cha Sheria ya a Haki za Binadamu.Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akizungumza  katika hafla fupi ya kusaini Makubaliano (MOU) juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.

Amesema makubaliano hayo yalipaswa kufanyika mwishoni mwa mwaka 2023 lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo  ilishindikana na kufanyika mwezi huu wa Januari ambapo makubaliano haya yatasaidia kuongeza na kuwajengea uelewa wapelelezi na Wachunguzi katika uendeshaji wa kesi zinazohusiana na usafirishaji wa haramu wa binadamu.

Mwakitalu amesema mahusiano ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Wanasheria Wasio na Mipaka (Laywers Without Borders) yameanza mwaka 2017 pale wanasheria kutoka taasisi ya Wanasheria Wasio na Mipaka walipotembelea ofisi ya Taifa ya Mashtaka na kuonyesha utayari wa kushirikiana kwa kutoa mafunzo kwa Waendesha Mashtaka ili kuwajengea uwezo mzuri wa kuendesha kesi zinazohusiana na usafirshaji haramu wa binadamu.

Katika hatua nyingine Mwakitalu amesema suala la Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu limekuwa tatizo kwa nchi nyingi, kanda na duniani kote hali ambayo, nguvu ya pamoja ya kupambana na tatizo hilo inahitajika.

Ameeleza kuwa Tanzania ni moja ya nchi zinazokabiliana na tatizo hilo   hivyo vita dhidi ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu ikiwemo hatua ya kutambua na kuchukua hatua kwa wale wanaobainika kuhusika na usafirishaji huu ambapo Serikali tayari inatekeleza Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu ya mwaka 2008.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la Kiserikali la Wanashria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders). Bi Robin Tylor amesema Makubalina hayo ina dhamira ya kuwaleta pamoja wadau wa mapambano dhidi ya biashara ya usafiriahaji haramu wa binadamu   kufanya kazi kwa pamoja na kuhakikisha wahalifu na magenge ya biashara hiyo wanafikishwa mbele ya vyombo vya dola na waathirika wa biashara hizo wanapata haki.

“Juhudi hizi zitafikiwa iwapo wadau wote tutaunganisha nguvu ya kupambana dhidi ya biashara hiyo ambayo ninaamini chini ya uongozi thabiti wa Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP) na kwa kusaini makubaliano haya malengo yatafikiwa”alisema Bi. RobinMkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lwayers without Borders) Bi. Robin Tylor akizungumza  katika hafla fupi ya kusaini Makubaliano juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.

Bi. Robin ameongeza kuwa kuna haja wadau kutumia sheria ya mapambano dhidi ya Usafirishaji wa Binadamu ya Mwaka 2008 iliyofanyiwa maboresho 2022 katika kuandaa Hati za Mashtaka pale wahalifu wanapokamatwa na wakati upelelezi na ushahidi kukamilika.

Bi Robin amehitimisha hotuba yake alisema kuwa, kwa sasa dunia iko katika matumizi ya teknolojia hivyo ni vema tukajikita katika kutumia teknolojia kwenye upelelezi na ukusanyaji wa vielelezo vya kesi zinazohusiana na biashara haramu na ulinzi wa waathirika na mashahidi wa biashara hiyo.

Wakati huo huo, Robin ameishukuru Serikali ya Marekani kupitia Ofisi ya Ufuatiliaji na Upambanaji wa Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu (J/TIP) kutoa ufadhili wa mradi huo.

Naye Mkuu wa Kikosi kazi ya Kukabiliana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu Tulibake Faidon Kasongwa amewashukuru wadau mbalimbali katika jitihada zao za kifedha na kimafunzo katika kuwajengea uwezo ndani ya Kikosi Kazi ambacho kimekuwa kikipambana na kuzuia Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu kwa kuwa wamekuwa chachu katika utendaji kazi wao.

Kasongwa amelishukuru Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) kwa  kuwajengea ujuzi wadau wa Haki Jinai ikiwa ni njia mojawapo ya ushirikiano na kuwawezesha kuwa na uwezo wa kuwajibika kwa haraka na kwa wakati  yanapotokea masuala ya biashara haramu ya binadamu.

Amesema kuwa biashara haramu ya binadamu ni janga la dunia  ambalo linahitaji ushirikiano wa wadau wote wa ndani na nje ya nchi  katika kukabiliana na dhuluma zinazofanyika kupitia biashara hiyo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini  Kamishna wa Polisi Salehe Ambika Mussa amesema suala la biashara haramu ya binadamu ni janga linalohitaji ushirikiano wa wadau wanaohitaji  kuunganisha nguvu za pamoja ili kuweza kuyafikia mafanikio kusudiwa.

Kamishna Mussa amebainisha kuwa licha ya kuwa na jukumu kubwa la kupeleleza kesi mbalimbali kwa niaba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuhakikisha haki inatendeka, suala la biashara  haramu ya binadamu ni jambo linalohitaji wadau wote kushirikiana na jeshi la polisi linapokuwa linafanya uchunguzi.

Mradi wa Kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu umeanza kutekelezwa mwezi Mei mwaka 2023 na  unatarajiwa kukamilika mwaka 2026.  Mradi huu umelenga katika kuwajengea uwezo Waendesha Mashtaka na Watekelezaji wa Sheria katika kuendesha Upelelezi, kuratibu ushahidi,na kuendesha Mashtaka ya Makosa ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu pamoja na kuimarisha ushirikiano wa kiutendaji katika mapambano ya Usafirshaji  Haramu wa Binadamu.Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Javelin Rugaihuruza akimkaribisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu kuzungumza katika hafla fupi ya kusaini Makubaliano juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.Kaimu Mkurugenzi wa Upelelezi Makosa ya Jinai Nchini Kamishna wa Polisi CP. Salehe Ambika Mussa akizungumza  katika hafla fupi ya kusaini Makubaliano juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.Tulibake Faidon Kasongwa  Mkuu wa Kikosi Kazi cha  Kukabiliana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu   akizungumza  katika hafla fupi ya kusaini Makubaliano juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu.Mkurugenzi Divisheni ya Utaifishaji Mali, Makosa yanayovuka Mipaka na Uhalifu Mahususi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bw. Faraja Nchimbi akizungumza  katika hafla fupi ya kusaini Makubaliano juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu  na  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lwayers Without Borders) Wakisaini Makubaliano (MOU) juu ya Utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu. Makubaliano hayo yamefanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu (kulia) akibadilishana Hati ya Makubaliano na  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lwayers Without Borders)  baada ya kusaini Makubaliano hayo (MOU) juu ya utekelezaji wa Mradi wa kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu katika hafla hiyo iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu kulia na  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lwayers Without Border) kushoto Wakionesha hati za Makubaliano (MOU) mara baada ya kusainiwa.Baadhi ya washiriki wa hafla ya kusaini Makubaliano juu ya utekelezaji wa Mradi wa wa Kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu wakifuatilia hotuba za Viongozi mbalimbali katika hafla hiyo iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza.Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu (kushoto) akikabidhiwa picha inayoonyesha ramani ya bara la Afrika na utajiri wa Wanyama pori pamoja na Picha ya Mchoraji wa Ramani hiyo kutoka kwa  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (Lawyers Without Borders) Bi. Robin Tylor.
Baadhi ya Wakuu wa  Mashtaka kutoka Mikoa mblimbali wakifuatilia hotuba za Viongozi  katika hafla ya kusaini Makubaliano (MOU) kati ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka (LWOB).Baadhi ya Watendaji kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtka wakifuatilia hotuba za Viongozi mbalimbali katika hafla ya kusaini Makubaliano kati ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka.

Baadhi ya Wakurugenzi Wasaidizi  kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtka wakifuatilia hotuba za Viongozi mbalimbali katika hafla ya kusaini Makubaliano kati ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na Shirika la Wanasheria Wasio na Mipaka.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa hafla ya kusaini Makubaliano juu ya utekelezaji wa Mradi wa wa Kukabiliana na Biashara ya Usafirishaji Haramu wa Binadamu katika hafla hiyo iliyofanyika tarehe 24 Januari, 2024 Jijini Mwanza


















 

 

Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .