• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

DPP AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA KUONGEZA BIDII KATIKA KAZI

 Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu amewataka watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  kuongeza bidii, jitihada na ubunifu katika kazi ili Ofisi hiyo iwe ni ofisi bora na pia iwe ni ofisi ambayo wananchi wanakimbilia kupata huduma na kupata haki yao.



Mkurugenzi Mwakitalu amebainisha hayo wakati alipokutana na kuzungumza na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kushiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (MeiMosi) yaliyofanyika leo tarehe 1 Mei, 2025 katika viwanja vya Bombadia Mkoani Singida.

Sambamba na hilo Mkurugenzi wa Mashtaka ametoa pongezi kwa watumishi hao kwa kujituma kufanya kazi vizuri na kuleta matokeo chanya katika taasisi hiyo.

"Nimepita baadhi ya mikoa na nimeona wananchi wanaamini wakija Ofisi ya Taifa ya Mashtaka watapata ufumbuzi wa matatizo yao." Ameyasema Mkurugenzi Mwakitalu

Share:

OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA YACHANGIA UFANISI KATIKA USIKILIZWAJI WA KESI ZA UHUJUMU UCHUMI NCHINI

 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, wakati akiwasilisha hotuba ya Bajeti  ya  Wizara hiyo kwa Mwaka 2025/2026 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,  Leo tarehe 30 April 2025  ameeleza kuwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imechangia ufanisi mkubwa katika uendeshaji wa kesi za Uhujumu Uchumi kwa kipindi kati ya Julai 2024 na Aprili 2025.

Kupitia hotuba yake, Dkt.  Ndumbaro amelieleza Bunge kuwa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  kwa kipindi cha mwaka wa Fedha  2024/2025 iliendesha kesi kubwa 177 katika Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi  ukilinganisha na Kesi 60 pekee zilizoendeshwa katika kipindi  kama hicho kwa mwaka 2023/2024.

Waziri Ndumbaro pia amebainisha kuwa katika Kipindi cha Julai 2024 hadi Aprili 2025, kesi za jinai 27,523 ziliendeshwa katika Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya, tofauti na kesi 25,037 zilizoendeshwa katika Mahakama hizo kwa kipindi  kama hicho kwa  mwaka wa fedha 2023/2024.

Ameeleza zaidi  kuwa, Wizara ya Katiba na Sheria kupitia Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeendelea kusogeza huduma kwa wananchi ngazi za Mikoa na Wilaya, ambapo katika kipindi cha mwaka 2024/2025 huduma hizo zimepelekwa kwenye mikoa yote 26 nchini pamoja na  Mikoa minne ya kimashtaka hivyo kufanya idadi ya  mikoa 30 inayopata huduma za Kimashtaka. Sambamba na hilo Waziri Ndumbaro amesema Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imefikisha huduma za mashtaka katika Wilaya 108 nchini.

Ameongeza kusema kuwa, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imekamilisha ujenzi wa majengo yake katika mikoa ya Manyara, Shinyanga, Katavi, Rukwa, Pwani na mkoa wa Kimashtaka Ilala.

Share:

"Uchunguzi wa Makosa ya kifedha ni nguzo muhimu sana katika mapambano dhidi ya uhalifu wa kiuchumi. Mhe." Rose Ebrahim

 Jaji Mfawidhi wa Mahamaka Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro Mhe. Rose Ebrahim amesema uchunguzi wa Makosa ya kifedha ni nguzo muhimu sana katika mapambano dhidi ya uhalifu huu wa kiuchumi kwani wahalifu wengi wa makosa hayo wamekuwa wakiibua mbinu mbalimbali za kidigitali ikiwemo kuunda mitandao tata isiyoshikwa kirahisi na mbinu za kawaida.

“Kwenye makosa ya kifedha wahalifu wengi huwa wanatumia mbinu za kiteknolojia kutenda au kuwezesha utendekaji wa makosa hayo, hivyo Wapelelezi na Waendesha Mashtaka lazima wawe na ujuzi wa kutosha kufaa kukusanya ushahidi wa kielektoniki na kufuata sheria zilizowekwa ili kusimama vyema bila kupoteza ushahidi”.

Mhe. Jaji ameyasema hayo wakati akifungua Mafunzo ya Utatu kuhusiana na Uchunguzi wa Makosa ya Kifedha na Uchunguzi wa Kisayansi yanayofanyika tarehe 25 na 26 Aprili, 2025 Mkoani Morogoro.

Jaji Mfawidhi amesema ni muhimu  mafunzo hayo kufanyika kwa kila mamlaka ili kuweka utaratibu wa kuwa na mafunzo endelevu ya kubaini mbinu zinavyobadilika kila kukicha kwani itasaidia kupata nafasi ya kubadilishana uzoefu kwa mambo au mbinu na changamoto ambazo wengine wanakutana nazo na namna bora ya kukabiliana nazo.

Katika hatua nyingine Mhe. Jaji amesisitiza juu ya umuhimu mkubwa wa Ushahidi wa Kisayansi katika utendaji wa haki ambapo Sayansi na Teknolojia vimeshika atamu.

“Ni lazima tuwe na maarifa na mbinu za kutosha za kiupelelezi na ukusanyaji ushahidi unaojibu makosa ya kifedha ili kuisaidia mahakama kutoa maamuzi yaliyosahihi kwa upande wa mashtaka na kuweza kutaifisha mali zinazotokana na makosa husika.’’ Amefafanua Mhe. Jaji Rose.

Sambamba na hilo amewataka Waendesha Mashtaka na Wapelelezi kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuwawezesha kupata ushahidi wa uhakika na uliokamilika.

Aidha, amesema Mashtaka bila ufuatiliaji wa mali ni ushahidi nusu, ni ushindi ambao bado haujakamilika. Uhalifu wa kifedha sio tu kuwafikisha wahusika mahakamani bali ni kuhusu Urejeshaji wa mali, uwajibikaji na kutoa fundisho kwa wengine.

Mali yoyote au fedha inayoporwa kutoka kwa umma au wananchi inapaswa kurejeshwa na kila mhalifu hanabudi ya  kuadhibiwa pamoja na kupokonywa faida ya uhalifu huo.

Pia amesema mafunzo hayo yakawe chachu kwao katika kupambana na uhalifu huo wa kifedha na kutumia ushahidi wa kisayansi ili kuhakikisha kuwa hakuna mtu yeyote atakaethubutu kuchezea mali za taifa, kuzipora au kuzihujumu na kuachwa akafaidika kwa namna yoyote ile.

Kwa upande wake Mkuu wa Mashtaka Mkoa wa Morogoro Bi. Tarsila Gervas ameeleza lengo la mafunzo hayo ni kuwaongezea uwezo Wapelelezi na Waendesha Mashtaka katika masuala ya Makosa ya kifedha pamoja na makosa mengine yanayohusisha Ushahidi wa Kisayansi.

Pia amesema mafunzo hayo ni dhamira ya dhati kwa Mkoa wa Morogoro katika kuhakikisha wanafanya upelelezi na uendeshaji wa mashtaka ambao unakuwa na ufanisi mkubwa na unaolenga kukomesha uhalifu katika mkoa huo.

"Tunataka kuujenga mkoa salama ambapo wananchi wake wanaweza kufanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii kwa amani pasipo kusumbuliwa wala kuwa uwoga wa vitendo vya kiuhalifu." Amefafanua Bi. Tarsila

Aidha mafunzo hayo yamehusisha taasisi mbalimbali zinazounda mnyororo wa haki jinai zikiwepo Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, TAKUKURU, TAWA, TANAPA, TFS, Jeshi la Polisi, na Uhamiaji.

Share:

DPP AWATAKA WAKUU WA MASHTAKA MIKOA KUIMARISHA UHUSIANO NA WADAU

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi  amewataka Wakuu wa Mashtaka wa Mikoa kuhakikisha wanaimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali wakiwemo wa haki jinai ili kuwezesha haki kupatikana kwa wakati.

Mkurugenzi wa Mashtaka ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano Maalum wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika tarehe 20 Machi, 2025 Mkoani Morogoro.

Akizungumza na wajumbe na washiriki wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mwakitalu amesema ni vema viongozi hao wakaimarisha ushirikiano kati yao na wadau wengine wakiwemo wadau wa haki jinai ili kurahisisha utendaji kazi wao.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi  Mwakitalu amewataka madereva wa Ofisi ya Mashtaka nchi nzima kufanya kazi zao kwa kuzingatia na kufuata Sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani.

Amesema   Madereva wasipozingatia  sheria, kanuni na utaratibu wa usalama Barabarani wawapo barabarani wanaweza sababisha ajali ambazo zinazuilika kwani  ajali husababisha hasara kubwa kwa Serikali, jamii na mtu mmoja mmoja.

‘’Kutofuatwa kwa sheria kunaweza kusababisha changamoto mbalimbali ikiwemo ajali, vifo, ulemavu, na kuharibika kwa mali ambayo serikali hutumia gharama kubwa kuzipata.” Amefafanua hayo Mkurugenzi Mwakitalu.

Aidha amewasisitiza watumishi kuendelea kufanya kazi zao kwa bidii ili kuyafikia mafaniko yaliyolengwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka katika kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa jamii vinadumu daima.

Wakati huo huo Baraza hilo limetumia nafasi hiyo kuwaaga watumishi waliostaafu utumishi wa umma katika Ofisi hiyo kwa kufikisha umri wa miaka 60 baada ya kulitumikia taifa ambapo Mkurugenzi Mwakitalu amewasisistiza kwenda kuyaishi mema waliyovuna wangali watumishi.

Wastaafu hao nao wameushukuru uongozi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka chini ya Mkurugenzi wa Mashtaka  kwa kuwashika mkono wakati wote na kuahidi kuzitumia vema fedha watakazolipwa kama kiinua mgongo.








Share:

BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA WATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA MIKUMI.

Wajumbe na washiriki wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza Bw. Sylvester Mwakitalu wamepata fursa ya kutembelea mbuga ya Wanyama ya Mikumi iliyopo Mkoa wa Morogoro ikiwa ni sehemu ya programu ya mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la kujadili na kupitisha Mpango wa bajeti  ya Ofisi  ya Taifa ya Mashtaka kwa Mwaka wa fedha 2025/2026.

Katika ziara hiyo wajumbe wamepata fursa ya kuona vivutio mbalimbali vya utalii ambavyo vinapatikana katika hifadhi hiyo vikiwemo Wanyama kama vile Simba, Nyumbu, Twiga, Pundamilia, Tembo na wengine wengi ambapo pia wamepata nafasi ya kujifunza mazingira, jiografia na mandhari  nzuri yaliyohifadhiwa na kutunzwa kupitia Mamlaka za Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).

Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya kuthamini jitihada na juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutangaza utalii wa Tanzania kupitia filamu ya The Royal Tour ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika kukuza sekta ya utalii ikiwemo kuhamasisha utalii wa ndani.





Share:

DPP NA MENEJIMENTI YA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA YAKUTANA MOROGORO KUJADILI MIKAKATI MIPYA YA UTENDAJI WA OFISI.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu ameendesha kikao kazi cha Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambacho kinafanyika Mkoani Morogroro kikilenga kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji, ikiwemo Maandalizi ya mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Tathmini ya utendaji kazi katika robo ya pili ya Octoba-Disemba 2024, Kupitia na kujadili rasimu ya sera ya Usalama  na Afya mahali pa kazi ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka. 

Kikao hiki kimefanyika tarehe 19 Machi, 2025 Mkoani Morogroro kikihusisha Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Simon Ntobbi, Wakurugenzi Wakuu wa Divisheni, Wakuu wa Vitengo na Wakurugenzi wasaidizi, ambapo kikao hicho kimelenga kuja na mstakabali mpya wa uendeshaji wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.




Share:

KIKAO CHA WELEDI BAINA YA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA NA WADAU

Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Rukwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Rukwa pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wamefanya kikao cha weledi pamoja na Semina kwa watumishi iliyotolewa kwa Madaktari waliopo katika mkoa huo.

Kikao hicho cha weledi kimefanyika tarehe 15 Machi, 2025 katika ukumbi wa Polisi wa Sumbawanga kwa lengo la kuongeza ujuzi na maarifa, kufanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuwahudumia wananchi kwa wakati na kufuata misingi ya haki iliyowekwa kisheria.

Katika kikao hicho mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwemo Elimu juu ya Uchukuaji wa Maelezo ya Onyo kwa njia ya Kimtandao, Uchoraji wa Ramani ya eneo la tukio pamoja na Ujazaji sahihi wa Polisi Fomu namba 3 (PF3), Vinasaba (DNA).

Aidha washiriki hao wameshukuru kwa kupata nafasi hiyo ya kujifunza na kubadilishana uzoefu, pia wameahidi ujuzi walioupata watautumia kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi na kuleta matokeo chanya.

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .