BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA WATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA MIKUMI.

Wajumbe na washiriki wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza Bw. Sylvester Mwakitalu wamepata fursa ya kutembelea mbuga ya Wanyama ya Mikumi iliyopo Mkoa wa Morogoro ikiwa ni sehemu ya programu ya mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la kujadili na kupitisha Mpango wa bajeti  ya Ofisi  ya Taifa ya Mashtaka kwa Mwaka wa fedha 2025/2026.

Katika ziara hiyo wajumbe wamepata fursa ya kuona vivutio mbalimbali vya utalii ambavyo vinapatikana katika hifadhi hiyo vikiwemo Wanyama kama vile Simba, Nyumbu, Twiga, Pundamilia, Tembo na wengine wengi ambapo pia wamepata nafasi ya kujifunza mazingira, jiografia na mandhari  nzuri yaliyohifadhiwa na kutunzwa kupitia Mamlaka za Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).

Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya kuthamini jitihada na juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutangaza utalii wa Tanzania kupitia filamu ya The Royal Tour ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika kukuza sekta ya utalii ikiwemo kuhamasisha utalii wa ndani.





Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .