Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu ameendesha kikao kazi cha Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambacho kinafanyika Mkoani Morogroro kikilenga kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji, ikiwemo Maandalizi ya mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Tathmini ya utendaji kazi katika robo ya pili ya Octoba-Disemba 2024, Kupitia na kujadili rasimu ya sera ya Usalama na Afya mahali pa kazi ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.
Kikao hiki kimefanyika tarehe 19 Machi, 2025 Mkoani Morogroro kikihusisha Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Simon Ntobbi, Wakurugenzi Wakuu wa Divisheni, Wakuu wa Vitengo na Wakurugenzi wasaidizi, ambapo kikao hicho kimelenga kuja na mstakabali mpya wa uendeshaji wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.






No comments:
Post a Comment