Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Rukwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Rukwa pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wamefanya kikao cha weledi pamoja na Semina kwa watumishi iliyotolewa kwa Madaktari waliopo katika mkoa huo.
Kikao hicho cha weledi kimefanyika tarehe 15 Machi, 2025 katika ukumbi wa Polisi wa Sumbawanga kwa lengo la kuongeza ujuzi na maarifa, kufanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuwahudumia wananchi kwa wakati na kufuata misingi ya haki iliyowekwa kisheria.
Katika kikao hicho mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwemo Elimu juu ya Uchukuaji wa Maelezo ya Onyo kwa njia ya Kimtandao, Uchoraji wa Ramani ya eneo la tukio pamoja na Ujazaji sahihi wa Polisi Fomu namba 3 (PF3), Vinasaba (DNA).
Aidha washiriki hao wameshukuru kwa kupata nafasi hiyo ya kujifunza na kubadilishana uzoefu, pia wameahidi ujuzi walioupata watautumia kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi na kuleta matokeo chanya.







No comments:
Post a Comment