• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

FANYENI KAZI KWA KUZINGATI HAKI NA USHIRIKIANO ILI KUFIKIA MALENGO YA NCHI-DPP MWAKITALU

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akihutubia katika hafla fupi ya ukaribisho wa kuanza kazi rasmi katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu  amewataka watumishi wa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kufanya kazi kwa kuzingatia Haki, Ushirikiano  kwa lengo la kusukuma gurudumu la maendeleo ya jamii na Taifa.

Bw. Sylvester amebainisha hayo mapema Mei 24, 2021 wakati akizungumza na viongozi na  watumishi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma alipowasili kwa mara ya kwanza tangu kuapishwa kwake.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester amewaasa Watumsihi wa Ofisi yake pale wanapoona wamekwama wasisite  kuhakikisha wanaomba ushauri ili kuweza kutatua changamoto zinazokwamisha  utekelezaji wa shughuli za  maendeleo.

“Niwaombe pale mtumishi unapoona ndivyo sivyo njoo tujadiliane ili kuweka mambo sawa, na mimi nitakapobaini tatizo kwenu, sitosita kukuita na kukurekebisha”

Mkurugenzi wa Mashtaka ameongeza kwa kuwataka watumishi wote wa Ofisi ya Taifa ya Mashataka kushikiriana pamoja ili kuwezesha kufikia lengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ikiwa ni pamoja na kutoa huduma bora kwa wananchi. 

“Niendelee kusema nanyi ndugu zangu watumishi wenzangu, tuna jukumu kubwa mbele yetu la kusimamia mashtaka lakini kubwa zaidi ni kutekeleza majukumu yetu kwa kuzingatia misingi ya sheria  na haki ambayo inapaswa kutendeka kwa wakati”

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande amesema kuwa ili kufikia malengo  yatakayofanikisha utaoji wa haki ni lazima wao kama waendesha Mashtaka wasimame kwa umoja na mshikamano hali itakayochangia kufikia malengo yao kwa wakati.

wakati huo huo Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu amekabidhiwa ofisi na aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka ambaye  sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe. Biswalo Mganga katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika Mei 25 Mei, 2021 katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande wakipokea maua ishara ya ukaribisho kwenye Ofisi ya Mashtaka kuanza utekelezaji wa Majukumu yao.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande kwa nyuma wakiingai rasmi Ofisii kuanza Majukumu yao.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akisaini kitabu cha wageni katika hafla fupi ya ukaribisho wao iliyofanyika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao makuu Jijini Dodoma
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande akisaini kitabu cha wageni katika hafla fupi ya ukaribisho wao iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao makuu Jijini Dodoma
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande akihutubia katika hafla fupi ya ukaribisho wa kuanza kazi rasmi katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma tarehe 24 Mei, 2021
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu (katikati),  Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma iliyofanyika tarehe 24 Mei, 2021.
Watumishi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu wakati akihutubia katika hafla fupi ya ukaribisho wao iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  Makao Makuu Jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande wakikata keki mara baada ya kukaribishwa katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka   Makao Makuu jijini Dodoma.
Watumishi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu wakati akihutubia katika hafla fupi ya ukaribisho wao iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka  Makao Makuu Jijini Dodoma
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu (katikati),  Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Mawakili  wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Makao Makuu Jijini Dodoma katika hafla ya ukaribisho wa kuanza kazi rasmi  iliyofanyika tarehe 24 Mei, 2021
 Tazama picha  mbalimbali katika tukio la Kuwasili kwa Mkurugenzi na Naibu Mkurugenzi wa Ofisi ya Taifa  ya Mashtaka  Makao Makuu Jijini Dodoma.



\


Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akisaini kitabu cha Makabidhianao ya Ofisi na  aliyekuwa Mkurugenzi wa Ofisi hiyo Biswalo Mganga ambaye kwa sasa ni Jaji wa mahakama ya Rufani nchini Tanzania 


Nakukabidhi Ofisi, endeleza  mapambano ya kuhakikisha  Mashauri yanaendeshwa kwa wakati. 

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Bi Rebeca Kwandu akiendelea kufuatilia na kusikiliza maneno ya Mkurugenzi Mashtaka wakati akikaribishwa na watumishi na wafanyakazi wa Ofisi hiyo Makao  Makuu Jijini Dodoma.
Share:

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AMUAPISHA MKURUGENZI WA MASHTAKA NAIBU MKURUGENZI NA WAKUU WA MIKOA JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu,hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Mei 19,2021 amewaapisha Viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni  wakiwemo, Mkurugenzi wa Mashtaka  Bw. Sylvester Mwakitalu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande, wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania bara hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha Wakuu Mikoa pamoja na  Watendaji wakuu wa Taasisi aliowateua Mhe. Rais Samia Suluhu amesema Uongozi ni kazi ya Mungu hivyo amewaasa kumtanguliza Mwenyezi Mungu wanapotekeleza majukumu yao.

Rais Samia amesema  Tanzania ina watu wasiopungua Milioni Sitini ambapo kati ya hao Milioni Kumi na tano wanazo sifa za kuwa Viongozi lakini wao ni miongoni mwa wachache waliofanikiwa kuteuliwa.

Awali Akizungumza katika tukio hilo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Philip  Isdory Mpango amewataka kila mmoja wa Viongozi walioteuliwa kufuata taratibu na kuheshimu Sheria sanjali na kuzingatia uongozi wa pamoja kwa kuwa ni wa muhimu sana

Dkt.Mpango amesema kuwa Kazi kubwa waliyonayo Wakuu wa Mikoa ni kusimamia uchumi wa Mikoa hususani kujielekeza kuongeza uzalishaji hasa kwenye kilimo lakini pia viwanda.

Aidha Dkt.Mapngo amewataka kwenda kushughulikia  masoko ya wananchi, hasa kukuza uchumi wa nchi ili kuwezesha upatikanaji wa maisha bora zaidi kwa wananchi

Kwa upande wake Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amewataka viongozi walioteuliwa  kuhakikisha wanafanya kazi kama timu na inapotokea kuwa kuna jambo linahitajika uwajibikaji basi.kuwepo na uwajibikaji wa pamoja.

Sisi pendekezo letu tuweke syncronization kati ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi ili kama Halmashauri hazitekelezi vizuri, wawajibike wote”amesema Mh.Job ndugai Spika wa Bunge

Mh. Ndugai amesema haiwezekani sheria itungwe kwamba asilimia 10 ya fedha iende kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, halafu zinakuja Halmashauri kadhaa ndani ya Mkoa uleule hazijatenga. Jambo ambalo linapaswa kuangaliwa kwa umakini

Naye Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amewaasa kujifunza na kutambua majukumu ya Taasisi walizopewa kuziongoza .

" Tambua majukumu ya Taasisi uliyopewa, jifunze nini kinachotakiwa kwenye ofisi yako, fahamu mipaka yako pamoja na kuwafahamu vizuri waliokuzunguka”amesema Kassim Majaliwa Waziri Mkuu .

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa  Ibrahim  Juma amesema DPP na TAKUKURU ni wadau muhimu katika mnyororo wa kusimamia na kutoa haki katika Mahakama ya Tanzania kwa sababu  DPP na TAKUKURU ni wadau muhimu sana wa Mahakama kwani  haki uanzia kwenye ngazi ya upelelezi na kuishia mahakamani. 

 "Tufanye kazi kama timu Inapotokea uwajibikaji tuwajibike wote RC, DC, RAS haipendezi inapotokea uwajibikaji haipendezi kuona Mkurugenzi anawajibika peke yake”amesema Profesa Juma Ibrahim Jaji Mkuu Tanzania.

Jaji Juma Ibrahim amesema ili haki ipatikane kwa wakati Upelelezi na uendeshaji wa Kesi ni lazima ufanyike kwa wakati hivyo aliitaka ofisi ya DPP na TAKUKURU kutembelea tovuti ya Mahakama ili kuangalia kesi zilizopo mahakani na muda zinazotakiwa kuisha ili waweze kuzifanyia kazi .

 " Tembeleeni tovuti ya Mahakama kuangalia wapi kuna tatizo. Endapo kesi imepitiliza muda iliyopangwa kuisha huwa tunaweka alama nyekundu ili muweze kuangalia wapi kuna tatizo na kurekebisha. Endapo kuna tatizo katika sheria  unaokwamisha  katika utoaji haki wasione haya katika kurekebisha sheria. Amesisitiza Profesa Juma Jaji  Mkuu.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw Sylvester Mwakitalu akila kiapo cha utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hayupo pichani) Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande akila kiapo cha utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hayupo pichani) Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.

Baadhi ya viongozi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka waliohudhuria hafla ya kuapishwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw Joseph Pande katika hafla ya kuwaapisha iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.





Share:

WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA NJOMBE

Washtakiwa watano waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji Kesi namba 84 ya mwaka 2014 ya Alice Mtokoma (56), mkazi wa Kijiji cha Usalule kilichopo Mkoani Njombe wamehukumiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa.

Wakisomewa shtaka hilo Machi 31, 2021 na wakili wa serikali Andrew Mandwa  na Matiko Nyangelo katika kikao cha Mahakama Kuu kilichofanyika mbele ya Jaji Firmin Matogolo walisema watuhumiwa hao Mei 13,  2012 walimuua  kwa kumpiga Alice Mtokoma kwa kitu chenye ncha kali, kosa ambalo ni kinyume na kifungu cha sheria namba  196 na 197, kanuni ya adhabu sura ya 16, marejeo ya 2019.

Wakili Nyangelo alieleza kuwa siku ya tukio hilo, watuhumiwa walimfuata nyumbani kwake marehemu na kumueleza kuna sehemu wanatakiwa kwenda naye ndipo walipotekeleza mauaji hayo.

Hukumu hiyo ya kunyongwa hadi kufa kwa washtakiwa hao ilitolewa na Jaji Matogolo katika kikao cha Mahakama Kuu kilichofanyika Mkoani Njombe.

Share:

RAIA 7 WA IRAN WAFIKISHWA MAHAKAMANI LINDI KWA KUSAFIRISHA HEROIN KILO 504.36

 Picha ya Dawa za Kulevya aina ya Heroin

RAIA  saba wa Iran akiwamo nahodha wa boti, Jan Miran (42) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi wakikabiliwa na mashtaka mawili ya kusafirisha heroin zenye uzito wa kilo 504.36 na Methamphetamine zenye uzito wa kilo 355.

Mbali na Miran, washtakiwa wengine ni Issa Ahmad(30), Amir Kasom (35), Salim Fedhmulhammad (20), Ikbal Mohammad(22), Mustaphar Bakshi (20) na Jawid Mohammadi(19).

Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao Aprili 30, 2021 na jopo la mawakili wa Serikali waandamizi,  Joseph Maugo na Juma Maige mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Maria Bantulayne.

Wakili Maige amedai washtakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 2/2021.

 Kabla ya kusomewa mashtaka yao, hakimu Bantulayne amesema washtakiwa hawatakiwi kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo ya uhujumu uchumi

Akiwasomea mashtaka yao, Wakili Maugo amedai katika shtaka la kwanza washtakiwa kwa pamoja wanadaiwa April 23, 2021 katika bahari ya Hindi eneo la Lindi wanadaiwa  kusafirisha heroin yenye uzito wa kilo 504.36

Katika shtaka la pili, siku na eneo hilo, washtakiwa hao wanadaiwa kusafirisha dawa za kulevya aina ya Methamphetamine yenye uzito wa kilo 355.0.

Hata hivyo washtakiwa hao walitafutiwa mkalimani anayejua Kiirani kutokana na wao kutokujua lugha nyingine.

Hakimu Bantulayne baada ya kusikiliza shauri hilo, aliahirisha kesi hadi Mei 14, 2021 itakapotajwa.

Washtakiwa wamerudishwa rumande kutokana na shtaka linalowakabili kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria.

kwa upande wake kamishna  wa  Tume ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA), Gerald Kusaya, ametangaza hali ya hatari kwa watu wote wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi, 

na kwamba wamejipanga kikamilifu na vita hivyo Tanzania inaenda kuishinda na kuwa na Tanzania huru bila ya dawa za kulevya.

Tumejipanga, tutatumia weledi, umakini, nyenzo na kushirikisha wadau wote, vyombo vyetu vya usalama,  kufanya kazi usiku na mchana, hatutalala na lazima tutakuwa washindi,” alisema Kusaya.

Aidha aliwataka raia wa Tanzania na wasio raia kutoa ushirikiano kwa Tume katika mapambano  akisisitiza kuwa ni vita ya wote ambayo haiwezi kufika mwisho isipokuwa pale kila mmoja atakapokuwa tayari kupambana.

Hii ni vita ya wote, nitoe rai kwa wananchi wote watoe taarifa na usiri ni jambo la muhimu kwa tume katika utekelezaji, wananchi watoe ushirikiano ili kushinda vita hii,” alisema.

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .