RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AMUAPISHA MKURUGENZI WA MASHTAKA NAIBU MKURUGENZI NA WAKUU WA MIKOA JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu,hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Mei 19,2021 amewaapisha Viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni  wakiwemo, Mkurugenzi wa Mashtaka  Bw. Sylvester Mwakitalu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande, wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania bara hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha Wakuu Mikoa pamoja na  Watendaji wakuu wa Taasisi aliowateua Mhe. Rais Samia Suluhu amesema Uongozi ni kazi ya Mungu hivyo amewaasa kumtanguliza Mwenyezi Mungu wanapotekeleza majukumu yao.

Rais Samia amesema  Tanzania ina watu wasiopungua Milioni Sitini ambapo kati ya hao Milioni Kumi na tano wanazo sifa za kuwa Viongozi lakini wao ni miongoni mwa wachache waliofanikiwa kuteuliwa.

Awali Akizungumza katika tukio hilo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Philip  Isdory Mpango amewataka kila mmoja wa Viongozi walioteuliwa kufuata taratibu na kuheshimu Sheria sanjali na kuzingatia uongozi wa pamoja kwa kuwa ni wa muhimu sana

Dkt.Mpango amesema kuwa Kazi kubwa waliyonayo Wakuu wa Mikoa ni kusimamia uchumi wa Mikoa hususani kujielekeza kuongeza uzalishaji hasa kwenye kilimo lakini pia viwanda.

Aidha Dkt.Mapngo amewataka kwenda kushughulikia  masoko ya wananchi, hasa kukuza uchumi wa nchi ili kuwezesha upatikanaji wa maisha bora zaidi kwa wananchi

Kwa upande wake Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amewataka viongozi walioteuliwa  kuhakikisha wanafanya kazi kama timu na inapotokea kuwa kuna jambo linahitajika uwajibikaji basi.kuwepo na uwajibikaji wa pamoja.

Sisi pendekezo letu tuweke syncronization kati ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi ili kama Halmashauri hazitekelezi vizuri, wawajibike wote”amesema Mh.Job ndugai Spika wa Bunge

Mh. Ndugai amesema haiwezekani sheria itungwe kwamba asilimia 10 ya fedha iende kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, halafu zinakuja Halmashauri kadhaa ndani ya Mkoa uleule hazijatenga. Jambo ambalo linapaswa kuangaliwa kwa umakini

Naye Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amewaasa kujifunza na kutambua majukumu ya Taasisi walizopewa kuziongoza .

" Tambua majukumu ya Taasisi uliyopewa, jifunze nini kinachotakiwa kwenye ofisi yako, fahamu mipaka yako pamoja na kuwafahamu vizuri waliokuzunguka”amesema Kassim Majaliwa Waziri Mkuu .

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa  Ibrahim  Juma amesema DPP na TAKUKURU ni wadau muhimu katika mnyororo wa kusimamia na kutoa haki katika Mahakama ya Tanzania kwa sababu  DPP na TAKUKURU ni wadau muhimu sana wa Mahakama kwani  haki uanzia kwenye ngazi ya upelelezi na kuishia mahakamani. 

 "Tufanye kazi kama timu Inapotokea uwajibikaji tuwajibike wote RC, DC, RAS haipendezi inapotokea uwajibikaji haipendezi kuona Mkurugenzi anawajibika peke yake”amesema Profesa Juma Ibrahim Jaji Mkuu Tanzania.

Jaji Juma Ibrahim amesema ili haki ipatikane kwa wakati Upelelezi na uendeshaji wa Kesi ni lazima ufanyike kwa wakati hivyo aliitaka ofisi ya DPP na TAKUKURU kutembelea tovuti ya Mahakama ili kuangalia kesi zilizopo mahakani na muda zinazotakiwa kuisha ili waweze kuzifanyia kazi .

 " Tembeleeni tovuti ya Mahakama kuangalia wapi kuna tatizo. Endapo kesi imepitiliza muda iliyopangwa kuisha huwa tunaweka alama nyekundu ili muweze kuangalia wapi kuna tatizo na kurekebisha. Endapo kuna tatizo katika sheria  unaokwamisha  katika utoaji haki wasione haya katika kurekebisha sheria. Amesisitiza Profesa Juma Jaji  Mkuu.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw Sylvester Mwakitalu akila kiapo cha utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hayupo pichani) Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Joseph Pande akila kiapo cha utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (hayupo pichani) Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.

Baadhi ya viongozi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka waliohudhuria hafla ya kuapishwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bw Joseph Pande katika hafla ya kuwaapisha iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Mei,2021.





Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .