KAIMU NAIBU MKURUGENZI WA MASHTAKA AISHUKURU UNICEF

 Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka ambae pia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji wa Kesi Bi. Neema Mwanda amelishukuru Shirika la Kimataifa la Watoto (UNICEF) kwa mchango wao mkubwa walioutoa katika kufadhili  Mafunzo na maelekezo ya utekelezaji wa ukaguzi  wa vizuizi vya watoto wanaokinzana na sheria wakishirikiana na timu ya maandalizi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambayo  yamefanyika leo tarehe 15 Novemba, 2021  katika Ukumbi wa Rafiki Hotel Jijini Dodoma.



"Elimu mnayopata hapa mkawape na wenzenu, msikae kimya kwani haitaleta tija katika utendaji wa kazi zetu. Na pia mkifika mkawe waalimu wa Mawakili wenzenu mliowaacha ili kesi za watoto ziweze kuendeshwa kwa ufanisi mkubwa na weledi."

Alizungumza hayo Bi. Neema Mwanda wakati akitoa neno la kufunga mafunzo hayo.


Nae pia Mratibu wa Ulinzi na Usalama wa Mtoto kutoka Shirika la Kimataifa la Watoto (UNICEF) Bi. Victoria Mgonela ametoa shukrani kwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na kueleza jinsi wanavyoshirikiana kikamilifu na ofisi hiyo katika kushughulikia mashauri ya watoto.

 


Share:

No comments:

Post a Comment

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .