• Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti

    Picha ya pamoja katika uzinduzi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti, Mugumu, mkoani Mara. ( Wa kwanza kushoto ni Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Bw. Edson Makallo baada ya kupokea taarifa ya magari yaliyotaifishwa kutokana na Uhujumu Uchumi na kuhifadhiwa katika kituo cha mabasi cha zamani jijini Dodoma.

  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka nchini

DPP AWATAKA WAKUU WA MASHTAKA MIKOA KUIMARISHA UHUSIANO NA WADAU

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi  amewataka Wakuu wa Mashtaka wa Mikoa kuhakikisha wanaimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali wakiwemo wa haki jinai ili kuwezesha haki kupatikana kwa wakati.

Mkurugenzi wa Mashtaka ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano Maalum wa Baraza la Wafanyakazi uliofanyika tarehe 20 Machi, 2025 Mkoani Morogoro.

Akizungumza na wajumbe na washiriki wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mwakitalu amesema ni vema viongozi hao wakaimarisha ushirikiano kati yao na wadau wengine wakiwemo wadau wa haki jinai ili kurahisisha utendaji kazi wao.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi  Mwakitalu amewataka madereva wa Ofisi ya Mashtaka nchi nzima kufanya kazi zao kwa kuzingatia na kufuata Sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani.

Amesema   Madereva wasipozingatia  sheria, kanuni na utaratibu wa usalama Barabarani wawapo barabarani wanaweza sababisha ajali ambazo zinazuilika kwani  ajali husababisha hasara kubwa kwa Serikali, jamii na mtu mmoja mmoja.

‘’Kutofuatwa kwa sheria kunaweza kusababisha changamoto mbalimbali ikiwemo ajali, vifo, ulemavu, na kuharibika kwa mali ambayo serikali hutumia gharama kubwa kuzipata.” Amefafanua hayo Mkurugenzi Mwakitalu.

Aidha amewasisitiza watumishi kuendelea kufanya kazi zao kwa bidii ili kuyafikia mafaniko yaliyolengwa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka katika kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa jamii vinadumu daima.

Wakati huo huo Baraza hilo limetumia nafasi hiyo kuwaaga watumishi waliostaafu utumishi wa umma katika Ofisi hiyo kwa kufikisha umri wa miaka 60 baada ya kulitumikia taifa ambapo Mkurugenzi Mwakitalu amewasisistiza kwenda kuyaishi mema waliyovuna wangali watumishi.

Wastaafu hao nao wameushukuru uongozi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka chini ya Mkurugenzi wa Mashtaka  kwa kuwashika mkono wakati wote na kuahidi kuzitumia vema fedha watakazolipwa kama kiinua mgongo.








Share:

BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA WATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA MIKUMI.

Wajumbe na washiriki wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza Bw. Sylvester Mwakitalu wamepata fursa ya kutembelea mbuga ya Wanyama ya Mikumi iliyopo Mkoa wa Morogoro ikiwa ni sehemu ya programu ya mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la kujadili na kupitisha Mpango wa bajeti  ya Ofisi  ya Taifa ya Mashtaka kwa Mwaka wa fedha 2025/2026.

Katika ziara hiyo wajumbe wamepata fursa ya kuona vivutio mbalimbali vya utalii ambavyo vinapatikana katika hifadhi hiyo vikiwemo Wanyama kama vile Simba, Nyumbu, Twiga, Pundamilia, Tembo na wengine wengi ambapo pia wamepata nafasi ya kujifunza mazingira, jiografia na mandhari  nzuri yaliyohifadhiwa na kutunzwa kupitia Mamlaka za Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).

Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya kuthamini jitihada na juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutangaza utalii wa Tanzania kupitia filamu ya The Royal Tour ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika kukuza sekta ya utalii ikiwemo kuhamasisha utalii wa ndani.





Share:

DPP NA MENEJIMENTI YA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA YAKUTANA MOROGORO KUJADILI MIKAKATI MIPYA YA UTENDAJI WA OFISI.

Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu ameendesha kikao kazi cha Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka ambacho kinafanyika Mkoani Morogroro kikilenga kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji, ikiwemo Maandalizi ya mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Tathmini ya utendaji kazi katika robo ya pili ya Octoba-Disemba 2024, Kupitia na kujadili rasimu ya sera ya Usalama  na Afya mahali pa kazi ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka. 

Kikao hiki kimefanyika tarehe 19 Machi, 2025 Mkoani Morogroro kikihusisha Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Simon Ntobbi, Wakurugenzi Wakuu wa Divisheni, Wakuu wa Vitengo na Wakurugenzi wasaidizi, ambapo kikao hicho kimelenga kuja na mstakabali mpya wa uendeshaji wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.




Share:

KIKAO CHA WELEDI BAINA YA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA NA WADAU

Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Rukwa kwa kushirikiana na Ofisi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Rukwa pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wamefanya kikao cha weledi pamoja na Semina kwa watumishi iliyotolewa kwa Madaktari waliopo katika mkoa huo.

Kikao hicho cha weledi kimefanyika tarehe 15 Machi, 2025 katika ukumbi wa Polisi wa Sumbawanga kwa lengo la kuongeza ujuzi na maarifa, kufanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuwahudumia wananchi kwa wakati na kufuata misingi ya haki iliyowekwa kisheria.

Katika kikao hicho mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwemo Elimu juu ya Uchukuaji wa Maelezo ya Onyo kwa njia ya Kimtandao, Uchoraji wa Ramani ya eneo la tukio pamoja na Ujazaji sahihi wa Polisi Fomu namba 3 (PF3), Vinasaba (DNA).

Aidha washiriki hao wameshukuru kwa kupata nafasi hiyo ya kujifunza na kubadilishana uzoefu, pia wameahidi ujuzi walioupata watautumia kutekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi na kuleta matokeo chanya.

Share:

AHUKUMIWA KUNYONGWA MPAKA KUFA


Mahakama Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Mtwara imemuhukumu Hamisi Peter Suwed @ Mkwidu (45) kunyongwa mpaka kufa baada ya kupatikana na hatia ya kosa la Mauaji ya Jamali Saidi Mtepa.

Hukumu hiyo imetolewa tarehe 13 Machi, 2025 na Jaji wa Mahakama hiyo Mhe. Martha Mpaze baada ya kusikiliza mashahidi watano (5) kutoka upande wa jamhuri pamoja na vielelezo vitano (5) na kujiridhisha kwamba upande wa Jamhuri umethibitisha shtaka pasipo kuacha shaka.

Katika kesi hiyo ya Kikao cha Jinai Na. 28 ya mwaka 2023  Bw. Hamisi am

baye ni mkazi wa kijiji cha Mavuji, Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi alikuwa anakabiliwa na shtaka la Mauaji kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Kanuni ya Adhabu, (Sura ya 16 Rejeo la mwaka 2022.) 

Mshtakiwa alitenda kosa hilo tarehe 25 Octoba, 2022 katika kijiji cha Mavuji, Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi ambapo inadaiwa kwamba, siku ya tukio majira ya usiku mshtakiwa wakati anarudi nyumbani kwake alimkuta marehemu akiwa anaiba mboga kwenye shamba lake, Mshtakiwa alichukua jiwe na kumpiga marehemu kichwani mara mbili mara baada ya hapo Mshtakiwa aliendelea kwa kuchukua kisu na kumchinja marehemu mpaka kupelekea kifo chake, pia mtuhumiwa alichukua mwili wa marehemu na kuutupa pembezoni mwa mto karibu na shamba lake.

Kesi hii imeendeshwa na jopo la Mawakili wa Serikali watatu kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka likiongozwa na Wakili Jordan Odhiambo akisaidiana na Denis Nguvu  pamoja na Hilal Kabyemela.

Share:

Labels

Recent Posts

MKURUGENZI WA MASHTAKA

MKURUGENZI WA MASHTAKA AWAONYA WANAOPANGA KUFANYA VURUGU ASEMA NCHI INAPASWA KUWA SALAMA WAKATI WOTE Contact me .